JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (9)

Katika sehemu ya nane, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alisema Rais ndiye aliyekiri kosa la Zanzibar kuingia katika OIC na pili ndiye aliyelazimika kukiri kule Dodoma kwamba utaratibu wa kushughulikia hoja ya Utanganyika ulikosewa lakini mawaziri wake mara zote mbili walitulia tu nakumuacha Rais ndiye akiri kosa na kubeba lawama. Ifuatayo ni sehemu ya kitabu cha Mwalimu Nyerere alichokiandika mwaka 1994 cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Endelea…

 

Katiba ya nchi yetu, na utaratibu tunaojaribu kujenga, vinataka kuwa katika hali kama hiyo, Mawaziri ndiyo wawajibike, na hivyo kumlinda Rais, si Rais awajibike, na kuwalinda Mawaziri wake, na tena  kwa kosa ambalo si lake. Watu walioshindwa uongozi Bungeni, hata tukafikishwa hapa tulipo leo, ni Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa CCM.

FASIHI FASAHA

Lissu ni malaika, waziri au mwanasiasa?


Ni takriban wiki tatu sasa tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kipate mtikisiko mkubwa, mithili ya pata shika na nguo kuchanika, baada ya Kamati Kuu (CC) ya chama hicho kuwavua nyadhifa zote viongozi wake watatu.

KONA YA AFYA

Sababu za kupungua nguvu za kiume -5


Wiki iliyopita, Dk. Khamisi Ibrahim Zephania alizungumzia kwa kina homoni ya kiume na umuhimu wake katika tendo la ndoa. Sasa endelea kumfuatilia zaidi…

Panahitajika ubongo, neva, homoni, mishipa ya damu, tezi [glands], utendaji mzuri wa figo, ini, baadhi ya misuli na viungo chungu nzima ndani ya mwili kama tutakavyoona katika makala zetu za mbele.

Milima, mabonde ya Nelson Mandela

 

Mpigania haki za weusi na alama kuu ya udhalimu wa mfumo wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, Mzee Nelson Madiba Mandela, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu, kutokana na maambukizo ya mapafu kushindwa kutengamaa.

Nyerere na Uhuru wa Tanganyika

Nazungumzia Uhuru wa Tanganyika. Sizungumziii Uhuru wa Tanzania Bara.

Majuzi niliona mabango yaliyosambazwa jijini Dar es Salaam. Mabango hayo yalisomeka “SHEREHE ZA MIAKA 52 YA UHURU WA TANZANIA BARA”.

Zuma: Nelson Mandela amepumzika kwa amani

Alhamisi usiku Desemba 5 mwaka huu, Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini,  alitangaza kifo cha Rais wa kwanza mweusi nchini humo, Nelson Mandela, ambaye amefariki dunia  akiwa na umri wa miaka 95.