JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

KAULI ZA WASOMAJI

Pongezi wana JAMHURI

Nawapongeza wafanyakazi wa Gazeti Jamhuri kwa kuanika wazi majina ya wauza unga katika toleo lililopita. Lakini kwanini serikali yetu isiwatie kitanzini kama huko China? Pia si hao tu, mafisadi nao watunguliwe risasi wazi wazi iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya uovu huo.

 

Justus Julius Mwombeki, Bukoba

0753 191 029

Wajasiriamali na mfupa wa huduma kwa wateja

Siku moja nilikuwa mjini Mafinga wilayani Mufindi katika Mkoa wa Iringa. Nikiwa hapo niliingia kwenye duka moja la vifaa vya ujenzi nikiwa na lengo la kununua vifaa kadhaa vyenye thamani ya takribani shilingi laki tatu.

Ponda naye anatafuta huruma ya waumini?

Mtakumbuka kuwa Agosti 10, mwaka huu, siku ya Idd Pili, iliisha vibaya kwa Katibu wa Jumuia na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda. Siku hiyo katika simu yangu uliingia ujumbe mmoja kutoka kwa watu zaidi 25. Ujumbe huo ulisomeka hivi ‘Sheikh Issa

Ponda amepigwa risasi Morogoro, wataarifu waumini wengine kumuombea na kukemea mashambulizi ya silaha dhidi yake’.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Tujifunze kusikiliza hoja za wengine

“Hatuna budi, hasa katika majadiliano na mazungumzo yanayohusu jumuiya, tujifunze kusikiliza hoja zilizotolewa na wenzetu, na kuzijibu kwa kuzikubali au kuzikataa, bila kujali kama aliyezitoa ni rafiki au si rafiki.”


Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Kwanza wa Tanganyika na baadaye Tanzania.

Dk. Mwakyembe sibipu, nakupigia mheshimiwa

Halo! Ni matumaini yangu kuwa uko hewani na unanisikia mheshimiwa. Nakuomba univumilie nimejiunga na mtandao wa Jamhuri kwa kuwa Voda, Tigo, Airtel na Zantel wameniambia salio langu halitoshi kuniwezesha niwe hewani kwa muda niutakao.

KONA YA AFYA

Misitu inavyoinufaisha Nanjilinji ‘A’ (3)

Mafanikio yaliyopatikana

Kijiji Nanjilinji ‘A’ kimedhihirisha kuwa iwapo wanavijiji watajipanga vizuri na kusimamia matumizi ya rasilimali ardhi na misitu ya asili katika vijiji, inawezekana kuboresha maisha yao. Kwa mtazamo wangu, Kijiji cha Nanjilinji ‘A’ kimekuwa mfano mzuri wa kuigwa na vijiji vingine vyenye rasilimali misitu, lakini misitu hiyo haitumiwi ipasavyo kwa faida ya wanakijiji. Kwa kipindi cha mwaka 2010/2011 kijiji kwa kushirikiana na MCDI kiliweza kupata soko la kuuza bidhaa za misitu hasa zitokanazo na mti aina ya mpingo.