Category: Makala
KAULI ZA WASOMAJI
Nasikitika vijana kukosa kazi
Ninasikitika kuona vijana wengi wasomi hapa Tanzania wakikosa kazi kwa muda mrefu baada ya kuhitimu masomo. Mikopo inayotolewa hairudishwi kwa wakati kwa sababu vijana hawana vyanzo vya mapato. Hivyo serikali itutafutie ufumbuzi wa tatizo hili kwa kasi, nguvu na ari mpya ili maisha bora kwa kila Mtanzania yapatikane.
Salim Habib, Morogoro
0652 054 343
Funga ya Ramadhani, hukumu, fadhila, adabu zake – 3
Katika sehemu ya pili ya makala haya, Sheikh Dk. Ibrahim Ghulaam, alizungumzia nyudhuru za funga, nguzo za funga, unavyothibiti kuingia Mwezi wa Ramadhani na yanayobatilisha funga. Sasa mfuatilie zaidi katika sehemu hii ya tatu…
Baadhi ya madereva hawajui matumizi taa za barabarani
“Mara nyingi ninapoendesha gari katika mitaa ya Jiji la Arusha, nalazimika kutumia akili nyingi. Hadi naondoka mjini huwa ninahisi uchovu wa kufanya kazi nzito ya kutumia akili.”
Serikali yaahidi kusaidia JKT
Julai 10, mwaka huu, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, aliwaoongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 50 ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Halmashauri ya Geita yatafunwa
* Sh mil 763.8 zakwapuliwa kifisadi
* Mwenyekiti CCM Mkoa ahusishwa
* Waandishi wa habari wapata mgawo
Siku chache baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa za nyaraka zinazoonesha Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilipokea Sh bilioni 11.1 za kununua madawati lakini fedha hizo hazijulikani zilivyotumika, taarifa nyingine zimepatikana zikionesha ubadhirifu wa Sh zaidi ya milioni 763 katika halmashauri.
Yah: Tanzania na maendeleo ya mdomo
Nianze kwa kuwashukuru sana wazazi wangu walionikanya wakati naoa kwamba maisha ya ndoa ni kama glasi ndani ya kabati, ipo siku lazima kabati litayumba na glasi zitagongana, na ikitokea hivyo katika maisha yangu ya ndoa lazima nitumie kuta nne za chumbani kwangu kumaliza kelele zetu za glasi, ugomvi na sintofahamu yoyote ile.