JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.

Nyalandu aweweseka siri kuvuja

*Aanza kuwasaka wabaya wake, awatisha Aprili 22, mwaka huu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akiwa na baadhi ya watendaji waandamizi wa Wizara hiyo mjini Dodoma, alitoa vitisho akiahidi kuwashughulikia wote aliodai kuwa wanavujisha siri za ofisi kwa watu…

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.
Vyanzo vya kuaminika vilivyopo karibu na Kipande, vinasema kwa sasa ameacha kumwamini kila mtu na hasa baada ya JAMHURI kupata habari za ndani ya kikao alichokuwa anatamba kuwa amemng’oa Mkurugenzi wa Masoko, Francisca Muindi, kitu ambacho hakutarajia kuwa kingelifikia gazeti hili.

Yah: Tusichezee lugha yetu, wengine wanajuta

Wakati tunatawaliwa, wakoloni wote kwa awamu zao yaani Wajerumani, Waingereza na hata Wareno na Waarabu, wakati wakipita kwa biashara zao sisi Wazaramo na Wandengereko tulikuwa tunawasiliana kwa shida sana. Kuna wakati tulikuwa tunatumia lugha ya alama kuwasiliana. Baada ya kuanza…

Fedha zako ni kipimo cha imani yako

Nianze kwa kuwasalimu wasomaji wetu. Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mchakato wa Katiba mpya, lakini ninasikitishwa na namna mwenendo wa Bunge hilo ulivyo.

Wiki iliyopita tumeshuhudia mgogoro wa kimakundi uliosababisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kususia vikao vya Bunge Maalum la Katiba.

Binafsi ninaamini kuwa pande zote zitakaa chini na kufikia mwafaka ili Taifa letu lipate Katiba mpya.

Sasa tuendelee na uchambuzi wa leo unaohusu uhusiano wa imani zetu na umilikaji fedha.

Tangu lini wapinzani wanawapenda wananchi?

Vyama vya upinzani vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) katika Bunge Maalum la Katiba vimesusia vikao vya bunge hilo tangu Aprili 16, mwaka huu.

Wapinzani wametoa sababu zao za kuchukua hatua hiyo. Kwa mfano, wamesema Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, wametoa vitisho kwamba kukiwapo Serikali tatu Jeshi litachukua nchi.