JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Hongera DC, Mahakama lakini sheria mbovu

WIKI iliyopita vyombo vya habari nchini vilichapisha habari kuwa Mahakama ya Wilaya Bunda imemtia hatiani na kuamuru afungwe jela miaka mitatu mfanyabiashara mwenye asili ya Kichina, Mark Wang Wei aliyejitoa wazi kumhonga Sh 500,000 Mkuu wa Wilaya hiyo, Joshua Mirumbe.

Ufisadi washamiri TTCL

*Mabilioni ya makusanyo yayeyuka

Wakati Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, January Makamba, alitarajiwa kukutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) jana, viongozi wakuu wake wanatuhumiwa kufanya ufisadi unaoiangamiza kampuni hiyo ya umma.

IGP Mwema heshima uliyoijenga inapotea

Miezi ya Desemba 2012 na Januari, 2013 imenitia hofu. Imenitia hofu baada ya kuwapo matukio mengi ya wizi, ujambazi na ukatiri dhidi ya binadamu. Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha wamelazimia kuandamana baada ya majambazi kuwa wanawavamia kwenye mabweni yao na kuwapora kompyuta za mkononi, fedha na vitu vya thamani. Imeelezwa kuwa hadi wanafikia uamuzi huo tayari walikwishaporwa laptop zipatazo 300.

TCRA kuvifungia vituo vya runinga

Siku za vituo vya runinga ambavyo havijajiunga na mfumo mpya wa dijitali nchini zinahesabika.

Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetangaza kuvinyang’anya leseni vituo hivyo ikiwa vitaendelea kukaidi agizo hilo la Serikali.

JAMHURI yafanikisha kukamatwa ‘majangili’

Wizara ya Maliasili na Utalii imewatia mbaroni watuhumiwa wa ujangili katika Kijiji cha Mkata, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.

Kashfa mpya Red Cross

*Dk. Nangale ‘achukua’ mitambo ya redio

Redio ya Sibuka imeingia katika kashfa nzito baada ya kubainika kuwa mitambo inayotumia redio hiyo kurusha mawimbi ya sauti ni mali Chama cha Msalaba Mwekundu (TCRS).