JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Maswi: Gesi imeanza kuwatajirisha Mtwara

“Kazi ya kuunganisha na kusambaza mabomba ya kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam imefikia hatua ya kuridhisha. Kazi hiyo inafanywa na  mashirika yenye uzoefu mkubwa kimataifa, ambayo ni Shirika la Teknolojia na Mendeleo ya Petroli la China (CPTDC), Kampuni ya Kutengeneza Mabomba ya China (CCP), Worley Parsons Limited na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Tayari mpaka sasa kilomita 142 kati ya 542 zimekamilika. Mradi huo unaotarajiwa kukamilika Desemba mwakani na utakuwa na mitambo ya kisasa.”

Yah: Mheshimiwa Kikwete: wananchi wanasema yatosha!

Salamu nyingi sana kama mchanga wa pwani zikufikie mahali popote ulipo, hofu na mashaka ni juu yako uliye mbali na upeo wa macho yangu, na baada ya salaam je hujambo.

Rais anasubiri nini kuifumua Wizara ya Elimu

kama tujuavyo imebaki miaka miwili Rais aliyepo madarakani Jakaya Mrisho Kikwete amalize muda wake kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tayari tumemsikia Rais Kikwete akijivunia utendaji wake Amesema kwamba wale walioendelea kumsema vibaya kwamba chini ya uongozi wake Tanzania haikupata maendeleo  wataoona aibu atakampomaliza muda wake. Atakuwa ameiacha Tanzania ikiwa na maendeleo yasiyo na kifani.

Mwarobaini hutibu mnyauko wa migomba

Mwarobaini ni mojawapo ya mimea maarufu yenye kinga dhidi ya wadudu waharibifu. Ndani yake kuna dawa inayoweza kutolewa kwa urahisi na kutayarishwa na kutumika kama dawa ya mimea ya kuulia wadudu.

Kinachonifanya nimpende Lowassa, hitimisho

Wakati naandaa makala niliyosema “Kinachonifanya nimpende Lowassa ni hiki” na kuichapisha katika gazeti hili la JAMHURI wiki iliyopita, hayakuwa mategemeo yangu kama makala hiyo ingeigusa jamii kwa kiasi nilichokishuhudia. Nimepigiwa simu nyingi mno, nimetumiwa ujumbe mfupi wa maandishi mwingi,  na bado mpaka sasa naendelea kupokea simu na ujumbe!

FASIHI FASAHA

Vyama vya upinzani ni vichanga? -4

Katika sehemu ya tatu ya makala haya wiki iliyopita, nilizungumza uchanga wa vyama vya siasa na malengo yao. Pia niligusia kauli iliyotolewa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, wakati wa Uchaguzi Mkuu 1995 kuhusu uwezo wa vyama vya upinzani kushinda katika uchaguzi mkuu wa 2015. Leo tunaendelea…

Hivi tunavyozungumza CCM na vyama vya upinzani kila kimoja kimo katika harakati ya kupanga mipango ya kushinda uchaguzi huo. CCM itafikisha miaka 38 na baadhi ya vyama vya upinzani vitafikisha miaka 23. Hapatakuwa tena na suala la uchanga wala watoto. Labda suala la utoto!