Latest Posts
Mradi wa Nyumba za Bei Nafuu Mchikichini Wazinduliwa
Zitauzwa kwa wananchi wa kawaida, Waziri Tibaijuka aimwagia sifa NHC Watanzania wasio na viwanja sasa hawana sababu ya kuendelea kuhangaikia changamoto hiyo kwa vile Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kujenga nyumba za kuishi kwa ajili ya kuwauzia kwa bei nafuu.
Hongera Jamhuri, mmethubutu, mmeonesha njia
Naanza kwa kusema chereko chereko na hongera, pia kwa kutamka ‘Congratulations and Celebrations’ kwa gazeti Jamhuri kutimiza mwaka tangu kuingia sokoni mnamo Disemba 6, 2011 hadi leo. Vilevile natoa heko kwa waandishi wa habari kuliendesha gazeti hili hadi sasa, kwa umakini na utulivu, ndani ya soko la usambazaji wa habari kwa jamii.
Labour yaanza kuchukua nchi rejareja
Mzee wa Kiraracha aliposhinda uchaguzi mdogo wa ubunge wa Temeke mwaka 1996 alisema ameanza kuichukua nchi kirejareja. Lyatonga Mrema alikuwa ndio ametoka kushindwa uchaguzi wa rais na William Benjamin Mkapa, ndipo ‘kihiyo’ akatokea pale Temeke akachukuliwa na maji ya fitna za kisiasa na uchaguzi ukaitishwa.
Yah: Nimeoteshwa ndoto ni nani rais ajaye?
Wanangu, leo najua ni Jumanne nyingine ambayo mtakuwa mnatafakari mustakabali wa maisha yenu baada ya kuwa kila siku inayopita mnaona nafuu ya jana. Haya yote yawezekana ni kutokana na kosa lenu la kupiga kura katika kumchagua kiongozi wako kuanzia ngazi ya tawi hadi juu kabisa.
Asanteni Watanzania, tumethubutu, tuungeni mkono
Wiki hii Kampuni ya Jamhuri Media Limited inaandika historia ya kipekee. Juni 28, 2011 kwa ushirikiano wa waandishi wa habari wanne, tulisajili kampuni ya Jamhuri Media Limited. Oktoba 5, 2011 tulipata usajili wa Gazeti Jamhuri. Desemba 6, tukachapisha nakala ya kwanza ya Gazeti Jamhuri. Ni wazi basi, kuwa wiki hii tunahitimisha mwaka mmoja na nusu wa kampuni kusajiliwa, lakini pia tunatimiza mwaka mmoja wa kuendesha Gazeti Jamhuri.
Butoto atamani maendeleo Kabilizi
“Nina karibia kustaafu na kutoka mjini nirudi kijijini nikaungane kimawazo na kivitendo na wananchi wenzangu kuikomboa Kata ya Kabilizi katika Jimbo la Muleba Kusini.’’