JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ahsante TMF, Kazi ipo kwetu

  Miongoni mwa habari zilizopamba gazeti hili leo ni taarifa ya Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF), kutoa ruzuku ya Sh. bilioni 1.7 kwa vyombo vya habari 16.Awali ya yote tunaupongeza mfuko huo kwa namna inavyoratibu shughuli zake na…

KWA HILI LA OKWI Yanga inahadaa mashabiki wake

Edgar Aggaba, mwanasheria wa Emmanuel Okwi, nyota wa soka wa kimataifa kutoka Uganda, hakufika Dar es Salaam kusimamia kesi ya mchezaji huyo wakati Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ilipojadili mkataba na usajili wake katika klabu ya Yanga.

Lovy Longomba Gwiji aliyetokea katika familia ya wanamuziki

“Mtoto wa nyoka ni nyoka.” Usemi huu wa wahenga unajionesha wazi kwa baadhi ya familia zilizojaaliwa kuwa na vipaji vikubwa.

Vipaji hivyo vinaweza kuwa vya kucheza mpira, muziki, kucheza sarakasi, riadha, ndondi n.k.

Warioba, Spika Sitta wateketeza Sh 100bil

MPAKA Jumamosi ya Oktoba 4, mwaka huu, Bunge Maalumu la Katiba Mpya litakuwa limetumia zaidi ya Sh 100 bilioni bila kupatikana kilichotarajiwa.
Fedha hizo, ni hesabu kuanzia Mei mosi, 2012 siku ambayo Tume ya Marekebisho ya Katiba ambayo ilikuwa na kazi ya kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya ilipoanza kazi rasmi.

Kila mtu ni mjasiriamali

Watu wengi huwa wananiuliza swali hili mara kwa mara, “Je, kila mtu ni lazima awe mjasiriamali?”

Nimekuwa nikiwajibu na leo ninataka kulijibu kwa namna nyingine na kwa upana. Ili kulijibu swali hili ninaomba nitumie Biblia kupata baadhi za rejea.

Uchafu waharibu mandhari ya mji wa Songea

Wananchi Manispaa ya Songea wameelezea wasiwasi wao kuhusu kukumbwa na milipuko wa magonjwa mbalimbali, kutokana na kukidhiri kwa uchafu katika maeneo mbalimbali yakiwamo soko kuu la mji buo.

Wakizungumza na JAMHURI kwa nyakati tofauti, wamesema miundombinu ya maji taka Soko Kuu la Songea ni mibovu. Mitaro ya mji huo imefurika na kutiririsha maji hovyo yanayosambaa kwenye maeneo ya wauza nyanya, vitunguu, samaki na dagaa.