Latest Posts
Udokozi bandarini ukomeshwe
Bandari ya Dar es Salaam ni mashuhuri katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. Bandari hii, kwa muda mrefu, imekuwa kitovu cha biashara kati ya Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na Kati zisizokuwa na bandari (land locked).
Kuchinja si tatizo, tatizo ni udini
Wiki hii nimelazimika kuandika tena mada hii. Nimeiandika mada hii baada ya kuona moto unazidi kusambaa nchi nzima. Tatizo lilianzia Kanda ya Ziwa kwenye mikoa ya Mwanza na Geita, likaenda Shinyanga, lakini sasa limehamia Tunduma.
Kwimba walilia maji safi
Mbunge wa Kwimba, Shanif Hirani Mansoor (CCM), amesema ameshaanza kushughulikia ujenzi wa mabwawa ya maji katika kata kadhaa jimboni humo.
Mchele wakosa soko Same
Wakulima wa mpunga wilayani Same mkoani Kilimanjaro, wameeleza kushangazwa na uamuzi wa Serikali kuruhusu uagizaji wa mchele kutoka nje ya nchi, wakati wao wamekosa wanunuzi wa tani 15,000 za bidhaa hiyo hapa nchini.
Mjue vizuri Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Aprili 13, mwaka 1922, safari ndefu ya maisha ya Mwalimu Kambarage Nyerere iliyochukua miaka 77 na miezi 6 ilianza Mwitongo kijijini Butiama, kilomita takribani 30 kutoka mji wa Musoma, mashariki mwa Ziwa Victoria lililoko kaskazini mwa Tanzania. Siku hiyo mvua kubwa ilinyesha. Mama Mgaya Nyang’ombe, aliyekuwa mke wa tano kati ya 23 wa Chifu Nyerere Burito wa Zanaki, alijifungua mwanae wa pili. Kwa desturi za kabila la Wazanaki, mtoto wa kike ama wa kiume aliyezaliwa siku ya mvua alipewa jina la KAMBARAGE (mzimu wa mvua).
Ridhiwani Kikwete atoa ya moyoni
Wiki iliyopita gazeti hili lilichapisha sehemu ya kwanza ya mahojiano kati ya Ridhiwani Kikwete (pichani) na JAMHURI. Leo tunakulete sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano hayo.
JAMHURI: Mitandao ya kijamii unaisoma? Unajisikiaje wewe na Mheshimiwa Kikwete mnavyoshambuliwa?
RIDHIWANI: Hivi vitu kwanza tumshukuru Mungu kwa sababu Mungu amewapa watu nafasi ya kusema. Mitandao hii inatoa nafasi ya kuwafanya watu watoe yaliyomo moyoni mwao. Taarifa iliyosomwa na Waziri Mkuu mwaka 2007 ilionesha CCM ilikuwa imefanikiwa kutekeleza asilimia 98 ya Ilani ya Uchaguzi. Kufikia mwaka 2009 ikawa imetekelezwa kwa asilimia 100.