Latest Posts
Tuukatae ushoga na ndoa za jinsi moja – 1
Siku za karibuni nchi za Afrika zimetamkiwa na wakubwa matajiri wa nchi za Magharibi kupokea tabia ngeni ya ushoga na ndoa za jinsi moja. Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, amediriki hata kutishia kunyima misaada kutoka Uingereza kwa nchi zile zitakazokataa siasa yake hiyo ya kutambua ndoa za jinsi moja.
Dar es Salaam ina viongozi wabovu sijapata kuona
Wiki hii jicho langu limekutana na kitu kinachoitwa mipango miji. Nimejipa muda wa kufikiri na kulinganisha matamanio yetu kama Watanzania juu ya tunachokiita miji safi na bora iliyopangiliwa. Ulinganisho huu nimeufanya ndani na nje ya nchi. Nimejaribu kuangalia miji ya mikoa kama Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Kagera na Dar es Salaam.
Serikali ni mtuhumiwa pekee kipigo cha Dk. Ulimboka
Mkononi nina Gazeti la JAMHURI (Julai 10-16, 2012) toleo Na. 33. Nimevutiwa na kichwa cha habari, ‘Dk. Ulimboka siri zavuja’. Nimevutiwa na habari hii kwa sababu ni moja ya mambo yanayoigusa jamii kwa sasa ikizingatiwa kuwa bado hali yake kwa walio wengi hatuijui, lakini pia mgomo wa madaktari bado unaendelea (naomba mgomo huo uishe ili tuweze kupata huduma).
Siri ya mafanikio yangu kiuchumi
Sasa nimeamini kuwa ‘la kuteleza haliwezi kutembea’ na ‘la kuvunda halina ubani’. Wiki mbili zilizopita niliandika makala yaliyokuwa na kichwa chahabari, ‘Je, machozi ya walimu yatamimina fedha mitaani?’
Mchechu: Tanzania si masikini
“Maelezo kwamba Tanzania ni nchi masikini yananikera. Imefika mahala wanasiasa wanadhani ili uwe kiongozi bora ni lazima ujiainishe kuwa unatatea masikini. Natamani tukose misaada kwa miaka mitano, tutapata akili na kutumia vyema utajiri tulionao. Hatustahili misaada kabisa maana nchi hii inao utajiri wa kutosha.”
Maneno haya ameyasema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, akiwaambia wahariri wa vyombo vya habari mjini Morogoro kuwa mawazo ya Watanzania yanapaswa kufikiria kufanya kazi zaidi badala ya kutegeshea misaada.
Uncle Tom naye atafukuzwa Yanga kama Timbe au Papic?
Msimu uliopita, Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake mitaa ya Twiga na Jangwani jijini iliyokuwa ikitetea ubingwa wake, ilifundishwa na makocha watatu kwa nyakati tofauti. Kwanza ilianza ligi hiyo, Agosti mwaka jana ikiwa na Sam Timbe, Mganda…