JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mwadui ni bora kuliko nyingine nchini – Julio

Kocha wa Timu  ya Soka  ya Mwadui ya mkoani Shinyanga, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ametamba kwamba timu hiyo itakuwa bora katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kuliko zote zinazoshiriki.

Akizungumza na JAMHURI hivi karibuni,  Julio amesema kuwa timu hiyo itatoa upinzani mkali kwa timu za Simba,  Yanga  na Azam FC.

“Simba na Yanga hakuna mpira pale bali kuna makelele, niliwahi kufundisha timu ya Kajumulo, sikuwahi kufungwa na Simba wala Yanga na hata sasa nikifanya usajili wangu hakuna timu ya kunifunga kati ya timu hizo,” amesema Julio na kuongeza:

Vituko vya DC Geita vyaongezeka – 3

DC adaiwa kumtisha Roboyanke

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyara, Makoye Roboyanke (CCM), ambaye inadaiwa alivuliwa madaraka hayo na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie, amedai kuwa Septemba 10, 2013 mchana akiwa shambani kwake kijijini hapo, alipokea simu ya vitisho kutoka kwa kiongozi huyo wa Serikali.

“Alijitambulisha kwa jina moja la Mangochie na kwamba ndiye Mkuu wa Wilaya ya Geita, akaniuliza jina langu nami nikamjibu… akaniuliza ninachofanya kwa wakati huo na kazi yangu hasa ni nini, nikamwomba arekebishe kauli, na baada ya kurekebisha kauli na kuniuliza maswali ya msingi nilimpa ushirikiano.

Marijani Rajabu: Jabali la Muziki lililozimika ghafla 

Marijani Rajabu kweli hatunaye tena hapa duniani, lakini kamwe wadau na wapenzi wa muziki wa dansi hapa nchini hawatamsahau.

Alikuwa miongoni mwa wanamuziki waliotoa mchango mkubwa wa maendeleo ya nchi kupitia tungo za nyimbo zake maridhawa, zilizokuwa zikiendana na wakati.

Machi 23, 2014 Marijani alitimiza miaka 18 tangu atangulie mbele ya haki. Nguli huyo alifariki Machi 23, 1995 na kuzikwa siku iliyofuata katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

Marijani alizaliwa Machi 3, 1955,  Kariakoo, Dar es Salaam. Kwa mapenzi yake Mungu, akamchukua akiwa na umri wa miaka 40.

KAGAME NI MTIHANI

Viongozi Maziwa Makuu waufanye kwa Uangalifu – 4

 

Tangu Kagame na RPF waitwae Rwanda ni wazi kuwa nchi hiyo inapokea fadhila za Washington DC kuliko nchi yoyote nyingine katika Maziwa Makuu.

Misaada ambayo inatoka Marekani na Uingereza kuelekezwa Kigali ni mingi na ya aina mbalimbali. Kwa hesabu rahisi misaada hiyo inafafanua ustawi wa uchumi wa Rwanda tunaouona leo.

JWTZ: Tunavifyeka vikundi vya waasi Congo

Baada ya ushindi dhidi ya Waasi wa March 23 (M23), Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na Majeshi ya Umoja wa Mataifa (MUNUSCO) limesema hakuna kikwazo chochote cha  kuwaondoa waasi wa ADF- NALU  na FDRL.

Ilikosewa kuruhusu UKAWA bungeni

Wiki iliyopita wanachama wa unaotajwa kuwa ni Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) walisusia kushiriki vikao vya Bunge Maalum la Katiba vinavyoendelea mjini Dodoma.

UKAWA hiyo inaundwa na wanachama wa vyama vya upinzani miongoni mwa wajumbe wanaounda bunge hilo lililokabidhiwa jukumu nyeti la kuwezesha upatikanaji wa Katiba bora ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.