Latest Posts
Kesho nataka kuwaamini polisi, nani anipe mwongozo?
Sitaki iwe mbali, bali mapema sana kesho asubuhi nataka nitii bilakushurutushwa na mtu yoyote maana wengine wameishasema kuwa wamechoka na mchoko wao wameishauhalalisha kwa kupitisha amri, amri ambayo mahakama imethibitisha kuwa ilikuwa amri ya iliyopungukiwa vigezo kutoka kwa mtoto wa mkulima.
Rais JK, orodha ya mapapa wa mihadarati imeyeyukia wapi?
Katika gazeti hili kuna barua iliyoandikwa na mmoja wa Watanzania walio kwenye magereza Hong Kong, kutokana na usafirishaji mihadarati.
Maghoba: Tanzania isipuuze vitisho vya Kagame
Mwanajeshi mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Frank Maghoba, ameitahadharisha Tanzania, akiitaka kutopuuza kauli ya vitisho inayodaiwa kutolewa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, dhidi ya Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Baadhi ya madereva hawajui matumizi taa za barabarani
“Mara nyingi ninapoendesha gari katika mitaa ya Jiji la Arusha, nalazimika kutumia akili nyingi. Hadi naondoka mjini huwa ninahisi uchovu wa kufanya kazi nzito ya kutumia akili.”
Serikali yaahidi kusaidia JKT
Julai 10, mwaka huu, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, aliwaoongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 50 ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Halmashauri ya Geita yatafunwa
* Sh mil 763.8 zakwapuliwa kifisadi
* Mwenyekiti CCM Mkoa ahusishwa
* Waandishi wa habari wapata mgawo
Siku chache baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa za nyaraka zinazoonesha Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilipokea Sh bilioni 11.1 za kununua madawati lakini fedha hizo hazijulikani zilivyotumika, taarifa nyingine zimepatikana zikionesha ubadhirifu wa Sh zaidi ya milioni 763 katika halmashauri.