Latest Posts
Ofisi ya Waziri Mkuu watumbua fedha dawa za kulevya
Vita dhidi ya dawa za kulevya inakuwa ngumu baada ya watendaji waliokabidhiwa jukumu la kudhibiti biashara hii haramu kuugeuza mradi, mpango wa kutoa matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya.
Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini mpango wa kutoa matibabu kwa watu walioathirika na dawa za kulevya unaojulikana kama Medication Assisted Treatment (MAT) uliopaswa kuanza Agosti, mwaka huu tayari umeanza kuhujumiwa.
JWTZ ngangari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liko tayari wakati wowote kupeleka vikosi vyake kulinda amani nchini Sudan Kusini.
Ujumbe wa Pluijm uzingatiwe
Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Soka ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, Hans Van Der Pluijm, ametema nasaha nzito kwa timu hiyo, ambazo zinastahili kuzingatiwa pia na klabu nyingine za soka hapa Tanzania. Akizungumza katika hafla ya kumuaga…
Mameneja Tanesco wanolewa kuhusu Mazingira
Kutokana na upungufu wa umeme unaoikabili nchi yetu ya Tanzania, tunategemea kuwa uwekezaji katika sekta ya nishati utaongezeka, hivyo kuibua changamoto nyingi za kimazingira, kiuchumi na kijamii.
Haya yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Mazingira Wizara ya Nishati na Madini, Gedion Kasege, hivi karibuni wakati akifungua semina ya siku tano iliyowahusisha mameneja wa Tanesco nchini ili kujifunza masuala ya uhifadhi wa mazingira (Strategic Environmental Impact Assesment), utwaaji wa ardhi, Sheria ya Mazingira na masuala ya jinsia katika sekta na jinsi ya kukabiliana nayo kuweza kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Tukatae ukatili dhidi ya albino (2)
Juma lililopita nilizungumzia chimbuko na dhana potofu zinazoendelea miongoni mwa jamii yetu kuhusu watu wenye ualbino. Leo naangalia masuala ya utu, afya, haki, matatizo na usalama wao.
“Watu wenye ualbino” kama wanavyotaka wao wenyewe kuitwa, na wasiitwe albino au zeruzeru kwa sababu majina hayo yanadhalilisha utu wao. Binafsi sioni kama kuna udhalilishaji juu yao.
Maneno hayo mawili ya Kiswahili na Kiingereza yote yanatoa maana ile ile moja ya kukosa rangi kamili ya mwili. Ni vyema ndugu zangu wayakubali majina hayo. Nasema ninawaomba wayakubali majina hayo.
Ugaidi Kenya utuimarishe kiulinzi
Wimbi la matukio yanayohusishwa na ugaidi limeendelea kuitesa nchi ya Kenya kwa kuua na kujeruhi watu, kuharibu mali mbalimbali na kuisababishia hasara kubwa.
Wiki iliyopita watu zaidi ya 10 waliripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa wakati wa milipuko miwili iliyotokea katika soko kubwa la nguo la Gikomba mjini Nairobi.
Huo ni mfululizo wa matukio kadhaa yanayohusishwa moja kwa moja na ugaidi likiwamo lililoshambulia kituo cha maduka ya kifahari cha Westgate jijini Nairobi.