Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Arusha

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilipata fursa adhimu ya kutembelewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa David Kihenzile(MB), katika Mkutano Mkuu wa 18 wa Tathmini ya Utendaji wa Sekta ya Uchukuzi. Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa AICC, Jijini Arusha.

Katika mkutano huo, Naibu Waziri aliipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika utoaji wa taarifa sahihi na za kuaminika za hali ya hewa, ambazo zimeendelea kusaidia kuboresha usalama na ufanisi katika sekta ya uchukuzi na kuwa taasisi yenye kuaminiwa na Watanzania.

Mkutano huo unafanyika kwa muda wa siku tatu, kuanzia tarehe 15 – 17 Desemba 2025 na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa mbalimbali wa sekta ya uchukuzi.