Rais John Magufuli akisaini kitabu wakati alipofika nyumbani kwa marehemu Jaji Robert Kisanga leo jijini Dar es Salaam.

…Akiongea katika msiba huo katika kuwapa pole wafiwa.  Kulia ni Mama Janeth Magufuli, mke wa rais.

…Akiwa na viongozi mbalimbali waliofika katika msiba huo.

Marehemu Jaji Kisanga (aliyesimama) enzi za uhai wake.

Rais John Magufuli na mkewe Mama Janeth leo wamefika nyumbani kwa marehemu Jaji Robert Kisanga kutoa pole kutokana na kifo cha jaji huyo kilichotokea Januari 23, mwaka huu katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam.  Pia wamepata fursa ya kuuaga mwili huo.

By Jamhuri