Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliyevaa Buti ya Kahawia akifinyanga tonge la ugali likiwa tayari kuelekea kwenye bakuli la mchuzi kutoeza
Rais Mstaafu akitoeza tonge la ugali kwenye bakuli la mboga

 

Pita pita yangu nikajikuta nimetokea kwenye page ya twitter ya Rais wetu Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete akiandika post na kuweka picha za yeye na wazee wakila ugali kwenye sahani moja na bakuli moja la mboga.

Mimi binafsi post yake nimeipenda kwani inaonesha huyu mheshimiwa ni mtu wa watu maana kuona Mtu aliyewahi kuwa rais kula chakula kwenye sahani moja na bakuli moja ni nadra sana hasa kwenye misiba ya viongozi kama level ya Rais wa Nchi.

Mara nyingi tunashuhudia vyakula vya kifahari na sahani za kisasa zikitumika kula chakula tena kila mmoja na sahaani yake.

Mimi nimejifunza kitu je wewe umejifunza nini????

 

By Jamhuri