JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Majaji wanaolinda wauza ‘unga’ wabainika

>>Gazeti hili sasa limeamua kuwataja kwa majina
>>Mahakimu nao wanawaachia mapapa kienyeji
>>Kigogo ofisi ya DPP, Mahakama Temeke, Kinondoni ni balaa

Mahakama kupitia baadhi ya majaji na mahakimu wasio waadilifu imebainika kuwa kikwazo kikubwa katika vita dhidi ya dawa za kulevya nchini, uchunguzi wa JAMHURI umebaini.Pamoja na Mahakama, Ofisi ya Mwendesha Mashitaka wa Serikali (DPP), nayo imelaumiwa kwa kufuta kesi katika mazingira ambayo hata mtu ambaye hakusoma sheria, anaweza kuyatilia shaka.

Wakati vyombo hivi vikikwamisha vita hii, lawama zimekuwa zikielekezwa kwa polisi na vyombo vingine vya usalama, ambavyo watendaji kazi wake wanafanya kazi usiku na mchana.

Waasi M23 wachapwa Goma

Brigedi ya Jeshi la Umoja wa Mataifa (MONUSCO) inayolinda amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, imewadhibiti waasi wa kundi la March 23 (M23). Brigedi hiyo inayojulikana kwa kifupi kama FIB, inaongozwa na Mtanzania, Brigedia Jenerali James Mwakibolwa. Kwa sasa imelidhibiti eneo la Goma.

BRN kuinua elimu nchini

Kiwango cha elimu Tanzania kinatarajiwa kupanda, baada ya Serikali kuzindua mpango wa kufanikisha Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now-BRN).

Fursa za uwekezaji nchini zawavutia Wajapan

Serikali ya Japani imekiri kuvutiwa na kuhamasishwa na fursa za uwekezaji zilizopo hapa nchini, hususan katika sekta ya nishati ambako imeonesha nia ya kuwekeza.

Ndugu wa Barlow wataka IGP Mwema awajibu

Ndugu wa aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow aliyeuawa kwa kupigwa risasi, wamesema wanataka majibu ya kina kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema.

JWTZ: Hizi ni rasharasha

*Wasubiri wenzao A. Kusini, Malawi zianze za masika

*Kamanda: Matumaini ya Wakongo ni makubwa mno

*Waziri wa Ulinzi asema hali za vijana nzuri

Brigedi ya Jeshi la Umoja wa Mataifa (UN) la Kulinda Amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO) inayoongozwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ipo salama na inajiandaa usiku na mchana kuhakikisha amani inarejeshwa katika eneo hilo.

Habari za uhakika zinaeleza kwamba operesheni rasmi inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu baada ya vikosi kutoka Afrika Kusini na Malawi, kuungana na wenzao wa JWTZ ambao tayari wapo eneo hilo.