Category: Siasa
Siri zavuja Bandari
Kipande abanwa Bandari
TCAA nako kwafukuta ufisadi
*Wakurugenzi wahariri Waraka wa Hazina
*Mbinu hiyo yawafanya walipane mamilioni
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), inakabiliwa na tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Fadhil Manongi, hadi wiki iliyopita bado alikuwa akiendelea na dhima za kiofisi licha ya muda wake wa kung’atuka kuwadia.
Wakati Manongi akijiandaa kuiacha ofisi hiyo, kumekuwa na malalamiko ya matumizi mabaya ya fedha miongoni mwa wakurugenzi ambao ni washirika wake.
Siku za Kipande bandarini zahesabika
*Ni baada ya kuthibitika anatumia vibaya jina la Rais Kikwete, Ikulu
*Amuagiza Mwakyembe amchunguze, wafuatilia kumtukana Balozi
* Mtawa, Gurumo nao wakana, Mwakyembe adaiwa kumwogopa
*Aendelea kukaidi maagizo ya Bodi, amng’oa rasmi aliyeomba kazi yake
Na Deodatus Balile
Siku za Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mzee Madeni Kipande (58), kuendelea kuwa madarakani zinazidi kuyoyoma baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na tabia yake ya kutumia jina la Rais kuhalalisha matendo yake yenye kukiuka sheria za utumishi wa umma.
Habari za uhakika kutoka Ikulu na kwa baadhi ya mawaziri waandamizi, zinasema Rais Kikwete baada ya kupata taarifa za Kipande kutumia vibaya jina lake, alichukia na kuamua kumwita Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, na kumpa maagizo mazito.
Hotuba ya Lissu iliyosababisha TBC1 ‘izimwe’
Aprili 12, mwaka huu, Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Tundu Lissu aliwasilisha maoni ya Wajumbe walio wachache katika Kamati Namba Nne kuhusu sura ya kwanza nay a sura ya sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakati akiwasilisha, Televisheni ya Taifa (TBC1) ilikata matangazo yake katika kile kilichotafsiriwa na wengi kuwa ni kuuepusha umma kupata maoni ‘makali’ yaliyomo kwenye hotuba ya Lissu. Kwa kuzingatia haki ya wananchi ya kupata habari, JAMHURI inawaletea hotuba hiyo neno kwa neno. Endelea
UTANGULIZI
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Sura ya Kwanza na Sura ya Sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (‘Rasimu’) ndizo msingi ambao Rasimu yote imejengwa juu yao. Wakati Sura ya Kwanza inagusa suala la muundo wa Muungano katika ibara moja tu kati ya ibara tisa, Sura yote ya Sita inahusu ‘Muundo wa Jamhuri ya Muungano.’ Suala la Muungano na hasa Muundo wake limetawala mjadala wa kisiasa na kikatiba wa Tanzania kwa zaidi ya miaka thelathini. Ndio maana katika waraka wake wa siri kwa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (‘CCM’), Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ya chama hicho imetamka kwamba “muundo wa Muungano ndiyo moyo wa Rasimu na ndiyo unaoamua ibara nyingine zikae vipi.”
Suala hili pia limetawala mchakato wa Katiba Mpya tangu ulipoanza miaka mitatu iliyopita. Kama alivyosema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Joseph Sinde Warioba wakati wa kuwasilisha Ripoti ya Tume yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar tarehe 30 Disemba, 2013: “Moja ya mambo ambayo yamejadiliwa sana na kwa hisia kali tangu Rasimu ya awali ilipotolewa … ni Muungano wa Tanzania. Jambo kubwa limekuwa juu ya muundo wa Muungano.”
Umuhimu wa suala hili unathibitishwa pia na uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum kuelekeza kwamba Kamati zake Namba Moja hadi Kumi na Mbili zianze kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita ya Rasimu. Haya ni maoni ya wajumbe walio wachache wa Kamati Namba Nne juu ya Sura hizi mbili.
Wakubwa wanavyotafuna Bandari
- Tanzania imeimarisha maendeleo na haki za kijamii
- Profesa Kairuki akumbukwa Mtanzania wa mwanzo kuanzisha hospitali binafsi
- Museven awasilia jijini Dar es Salaam
- Rais Samia atekeleza ahadi ya wanawake, vijana ndani ya siku 100
- RC Chalamila : Wamachinga achieni njia za kuingia soko la Kariakoo kabla ya Februari 8
Habari mpya
- Tanzania imeimarisha maendeleo na haki za kijamii
- Profesa Kairuki akumbukwa Mtanzania wa mwanzo kuanzisha hospitali binafsi
- Museven awasilia jijini Dar es Salaam
- Rais Samia atekeleza ahadi ya wanawake, vijana ndani ya siku 100
- RC Chalamila : Wamachinga achieni njia za kuingia soko la Kariakoo kabla ya Februari 8
- Rais Samia afanya mabadiliko ya muundo wa wizara na uteuzi wa viongozi
- Serikali yasajili anwani za makazi milioni 12.9
- Dk Nchimbi ashiriki hafla ya kusimikwa kwa uongozi wa makanisa ya kipentekoste Tanzania
- Rais Samia ahitimisha ziara ya kikazi UAE, aimarisha mahusiano na uwekezaji
- Balozi Mwamweta, Mtaka wasaka soko la parachichi Ujerumani
- Shemdoe awataka madiwani kuwa wanyenyekevu kwa wananchi
- Serikali yaipongeza IAA kwa kuongoza mageuzi ya kidigitali na kusukuma utafiti na maendelo
- Wakurugenzi ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano
- TRA yawataka walipa kodi Morogoro kuuzoea mfumo mpya wa Idras
- Waziri Mkuu achukizwa na migogoro ya ardhi
Copyright 2025