JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Siri zavuja Bandari

 

*Orodha ndefu ya watumishi aliowaonea Kipande yatajwa
*Wafanyakazi wambatiza ‘Last King of Scotland’ – Idi Amin
*Takukuru yachunguza unyanyasaji huu, malipo mishahara
*Aliyerejeshwa kwa nguvu ya wakubwa apanga kumhamisha
*Mgogoro wazidi kutanuka, amsukia zengwe mshindani kazini
*Yeye, Mwakyembe, wabunge wiki watumia Sh milioni 360
Na Deodatus Balile
Siri nzito zimeanza kuvuja jinsi Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mzee Madeni Kipande (58), anavyofanya unyanyasaji kwa wafanyakazi wa Bandari hiyo, hasa wanawake, vyanzo vimeifahamisha JAMHURI.

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.

TCAA nako kwafukuta ufisadi

*Wakurugenzi wahariri Waraka wa Hazina

*Mbinu hiyo yawafanya walipane mamilioni

 

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), inakabiliwa na tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Fadhil Manongi, hadi wiki iliyopita bado alikuwa akiendelea na dhima za kiofisi licha ya muda wake wa kung’atuka kuwadia.

Wakati Manongi akijiandaa kuiacha ofisi hiyo, kumekuwa na malalamiko ya matumizi mabaya ya fedha miongoni mwa wakurugenzi ambao ni washirika wake.

Siku za Kipande bandarini zahesabika

*Ni baada ya kuthibitika anatumia vibaya jina la Rais Kikwete, Ikulu

*Amuagiza Mwakyembe amchunguze, wafuatilia kumtukana Balozi

* Mtawa, Gurumo nao wakana, Mwakyembe adaiwa kumwogopa

*Aendelea kukaidi maagizo ya Bodi, amng’oa rasmi aliyeomba kazi yake

Na Deodatus Balile

Siku za Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mzee Madeni Kipande (58), kuendelea kuwa madarakani zinazidi kuyoyoma baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na tabia yake ya kutumia jina la Rais kuhalalisha matendo yake yenye kukiuka sheria za utumishi wa umma.

Habari za uhakika kutoka Ikulu na kwa baadhi ya mawaziri waandamizi, zinasema Rais Kikwete baada ya kupata taarifa za Kipande kutumia vibaya jina lake, alichukia na kuamua kumwita Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, na kumpa maagizo mazito.

Hotuba ya Lissu iliyosababisha TBC1 ‘izimwe’

Aprili 12, mwaka huu, Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Tundu Lissu aliwasilisha maoni ya Wajumbe walio wachache katika Kamati Namba Nne kuhusu sura ya kwanza nay a sura ya sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wakati akiwasilisha, Televisheni ya Taifa (TBC1) ilikata matangazo yake katika kile kilichotafsiriwa na wengi kuwa ni kuuepusha umma kupata maoni ‘makali’ yaliyomo kwenye hotuba ya Lissu. Kwa kuzingatia haki ya wananchi ya kupata habari, JAMHURI inawaletea hotuba hiyo neno kwa neno. Endelea

UTANGULIZI

Mheshimiwa Mwenyekiti,

Sura ya Kwanza na Sura ya Sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (‘Rasimu’) ndizo msingi ambao Rasimu yote imejengwa juu yao. Wakati Sura ya Kwanza inagusa suala la muundo wa Muungano katika ibara moja tu kati ya ibara tisa, Sura yote ya Sita inahusu ‘Muundo wa Jamhuri ya Muungano.’ Suala la Muungano na hasa Muundo wake limetawala mjadala wa kisiasa na kikatiba wa Tanzania kwa zaidi ya miaka thelathini. Ndio maana katika waraka wake wa siri kwa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (‘CCM’), Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ya chama hicho imetamka kwamba “muundo wa Muungano ndiyo moyo wa Rasimu na ndiyo unaoamua ibara nyingine zikae vipi.”

Suala hili pia limetawala mchakato wa Katiba Mpya tangu ulipoanza miaka mitatu iliyopita. Kama alivyosema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Joseph Sinde Warioba wakati wa kuwasilisha Ripoti ya Tume yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar tarehe 30 Disemba, 2013: “Moja ya mambo ambayo yamejadiliwa sana na kwa hisia kali tangu Rasimu ya awali ilipotolewa … ni Muungano wa Tanzania. Jambo kubwa limekuwa juu ya muundo wa Muungano.”

Umuhimu wa suala hili unathibitishwa pia na uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum kuelekeza kwamba Kamati zake Namba Moja hadi Kumi na Mbili zianze kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita ya Rasimu. Haya ni maoni ya wajumbe walio wachache wa Kamati Namba Nne juu ya Sura hizi mbili.

Wakubwa wanavyotafuna Bandari

*Waanzisha EPA mpya, Bandari waitengea CCM bilioni 10
*Kinana aukana mradi, walipanga kujenga yadi ya malori
*Dk. Mwakyembe ampa onyo Kipande, agoma kuhojiwa
*Ikulu yakana kumlinda, wakili adai milioni 205/- kwa siku
*Mkurugenzi anyanyasa wanawake, Bodi ‘imewapotezea’
*Wataalamu waacha kazi TPA, Magesa akiri hakuna ulinzi

Utaratibu wa baadhi ya wanasiasa kuchota mabilioni ya shilingi kutoka kwenye Hazina ya Taifa kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu umeendelea.
Wakati mwaka 2005 zilitumika kampuni kama Kagoda, Deep Green na nyingine kuchota mabilioni ya EPA, zamu hii Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wameanzisha mradi kama huo kwa ajili ya mwaka 2015, ambapo wameitengea CCM Sh bilioni 10 kwa ajili ya mradi wa kuegesha magari.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Bandari, ambazo gazeti JAMHURI limezithibitisha, bajeti ya Mamlaka ya Bandari inaonesha kuwa wajanja wametumia kampuni tanzu ya CCM (SUKITA) Sh bilioni 10 kama kianzio kwenye bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya mradi wa kuegesha malori.
Mradi huu umeingizwa kiujanja kupitia Kampuni ya Lori Parking Yard kwenye Bonde la Msimbazi, eneo la Tabata Matumbi yaliko majengo ya SUKITA. JAMHURI imeshuhudia pilikapilika za ujenzi katika eneo hilo.
“Huwezi kuamini, huu ni mradi hewa. Wanatafuta fedha za Uchaguzi Mkuu mwaka 2015. Kwenye bajeti ya 2014/2015 wanasema kiasi cha Sh bilioni 10 kilichotengwa ni cha kuanzia. Mwakani kitatengwa kiasi kikubwa zaidi. Lakini ukiangalia uhalisia, hata kama kweli wangekuwa wanajenga maegesho ya malori, eneo hili haliruhusu uwepo wa maegesho haya.
“Pale Tabata ni katikati ya jiji kwa sasa, tuna msongamano mkubwa wa magari kuelekea kwenye makutano ya Ubungo, leo unasema unaweka yadi ya kuegesha malori Tabata! Utatengeneza msongamano wa kiasi gani? Kama ni yadi ya malori ilipaswa kujengwa hata nje ya Kibaha kuelekea karibu na Mlandizi, ila si katikati ya jiji. Lakini tunaojua, tunasema wajinga ndiyo waliwao. Ni mradi wa uchaguzi,” kilisema chanzo chetu.