JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Mangula kazima moto kwa petroli Bukoba

Kwa karibu miezi sita sasa, siasa za Jimbo la Bukoba mjini zimegeuzwa siasa za chuki, kutishana, fitina, kuchambana, kulaumiana, kuonesha umwambwa, uwezo wa kifedha, dharau, ubaguzi  na ujenzi wa matabaka yanayosigana katika jimbo hili.

Vinara mgogoro wa gesi watajwa

Matajiri wakubwa nchini wanaojihusisha na biashara ya mafuta ya petroli, mafuta mazito ya viwandani na kampuni kubwa za kimataifa, ni miongoni mwa wanaochochea mgogoro wa kupinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam , JAMHURI imethibitishiwa.

TAKUKURU yawahoji watuhumiwa TTCL

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imeanza rasmi kazi ya kuwahoji viongozi juu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Ufisadi washamiri TTCL

*Mabilioni ya makusanyo yayeyuka

Wakati Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, January Makamba, alitarajiwa kukutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) jana, viongozi wakuu wake wanatuhumiwa kufanya ufisadi unaoiangamiza kampuni hiyo ya umma.

TCRA kuvifungia vituo vya runinga

Siku za vituo vya runinga ambavyo havijajiunga na mfumo mpya wa dijitali nchini zinahesabika.

Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetangaza kuvinyang’anya leseni vituo hivyo ikiwa vitaendelea kukaidi agizo hilo la Serikali.

Ukabila watikisa Uhamiaji

*Wafanyakazi wamwandikia Waziri waraka

*Waorodhesha majina 70 ya wanaowatuhumu

*Mkutano wa wafanyakazi waitishwa, waonywa

Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji walioficha majina, wamemwandikia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. John Nchimbi, waraka wakilalamikia vitendo vya ukabila ndani ya Idara hiyo. Katika waraka huo, wamedai kwamba karibu nafasi zote nono zimeshikwa na makabila mawili pekee yanayotoka Mkoa wa Kilimanjaro.