JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Mtikisiko mkubwa CCM

*Msekwa, Karume kutemwa rasmi, vigogo wengi kuangukia pua

*Wasira, Lukuvi, Membe, Makamba, Mukama wapambana

*Balozi Seif, Shamsi, Khatib, Mbarawa, Samia, Mwinyi vita kali

Wiki hii Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha safu zake za uongozi, huku mtikisiko mkubwa ukitarajiwa kutokea kwa vigogo wengi kubwagwa kwenye nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) – viti 10 Bara na viti 10 Zanzibar.

Polisi wampuuza Kikwete

*Amri yake ya mwaka 2006 yaota mbawa

Jeshi la Polisi limepuuza agizo halali la Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, lililolitaka lihakikishe linawasomesha watoto watatu wa askari polisi, PC Abdallah Marwa.

Upendeleo watoto wa wakubwa

 

*Watoto wengine wa vigogo wajazwa Idara ya Afya

*Washika nafasi zote za Jiji, Ilala, Temeke, K’ndoni

Siku chache baada ya kuibuka mjadala wa kuwapo watoto wengi wa vigogo ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hali kama hiyo imejitokeza tena kwenye Idara ya Afya katika Jiji la Dar es Salaam na manispaa zake tatu za Temeke, Ilala na Kinondoni, JAMHURI imebaini.

Vigogo wagawana viwanja

Utapeli wa kutisha umefanywa na uongozi wa Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam, juu ya uuzaji viwanja katika eneo la Gezaulole.

BoT yajaa watoto wa vigogo

Wamo Salama Ali Hassan Mwinyi, Filbert Tluway Sumaye, Zaria Rashidi Kawawa, Blasia William Mkapa, Harriet Matern Lumbanga, Pamela Edward Lowassa, Rachel Muganda, Salma Omar Mahita, Justina Mungai, Kenneth Nchimbi, Violet Philemon Luhanjo, Liku Kate Kamba, Thomas Mongella na Jabir Abdallah Kigoda.

 

‘Kikitokea chama kama CCM ya Nyerere kitatawala milele’

Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alidhamiria kuifanya Tanzania kuwa paradiso.

“Mwalimu alitaka kujenga paradiso ya hapa duniani katika nchi hii. Kama tungetekeleza misingi aliyotuwekea, Tanzania ingekuwa paradiso.” Haya ni maneno ya Ibrahim Kaduma (75).

Kaduma ameshika nyadhifa mbalimbali, zikiwamo za ukurugenzi na uwaziri katika Serikali ya Awau ya Kwanza.