Category: Maoni ya Mhariri
Mchechu NHC ameonyesha njia, wakurugenzi wengine mko wapi?
Wiki iliyopita Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limepata mkopo wa wastani wa Sh bilioni 165. Shirika limeupata mkopo huu kutoka benki na mashirika tisa ya fedha. Mashirika na benki zilizotoa mkopo huu na kiasi cha fedha walizotoa kwenye mabano ni CRDB Bank (Sh 35 bilioni), ECO Bank (Sh 20 bilioni), ABC (Sh 4 bilioni), NMB (Sh 26 bilioni), CBA (Sh 24 bilioni), TIB (Sh 22 bilioni), Azania (Sh 7 bilioni), Local Authorities Pension Fund-LAPF (Sh 15 bilioni) na Shelter Africa Company (Sh 22 bilioni).
Bila reli, barabara zitakufa
Wizara ya Ujenzi, kama zilivyo wizara nyingine, ni miongoni mwa wizara chache ambazo ni mihimili ya maendeleo ya taifa letu.
Tanzania, tofauti na makoloni mengine, iliachwa na watawala dhalimu ikiwa haina barabara, si za lami tu, bali hata za changarawe.
Mabavu hayatanzuia mgomo wa madakatri
Kwa wiki nzima sasa nchi yetu imekumbwa na mgogoro mkubwa unaohusisha madaktari na serikali kwa upande mwingine.
Ukuaji wa deni la taifa udhibitiwe
Miaka mitatu iliyopita, deni la taifa lilikuwa Sh trilioni tano hivi, lakini mwaka huu wa 2012 deni hilo limepanda hadi kufikia zaidi ya Sh trilioni 20.
Wabunge waibane Serikali bila woga
Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.
Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kufanyika kwa kikao hicho kulikuwa ni maandaizi ya kuwaweka sawa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi, waweze kuipitisha bajeti hiyo. Hilo ni jambo la kawaida katika mabunge, hasa yenye mseto wa wabunge wanaotokana na vyama vingi vya siasa.
Tujiepuke bejeti kiinimacho
Wiki hii Serikali inatarajiwa kuwasilisha bajeti bungeni mjini Dodoma. Bejeti hii inakisiwa kuwa ya wastani wa shilingi trilioni 15. Hili ni ongezeko la wastani wa trilioni 2 kutoka trilioni 13 za mwaka jana. Kiasi hiki ni kikubwa mno kwa takwimu. Kinawafanya Watanzania kuwa na matumaini makubwa ila yapo yanayotusikitisha.