JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

FASIHI FASAHA

Miaka 50 hakuna maendeleo! – 2

Wiki iliyopita katika makala haya nilikumbusha vitu vinne: Ardhi, watu, siasa safi na uongozi bora jinsi vilivyoweza kuleta maendeleo ya nchi na watu katika elimu, afya, siasa na uchumi, pamoja na kujenga umoja na mshikamano wa Watanzania.

KAULI ZA WASOMAJI

Nasikitika vijana kukosa kazi

Ninasikitika kuona vijana wengi wasomi hapa Tanzania wakikosa kazi kwa muda mrefu baada ya kuhitimu masomo. Mikopo inayotolewa hairudishwi kwa wakati kwa sababu vijana hawana vyanzo vya mapato. Hivyo serikali itutafutie ufumbuzi wa tatizo hili kwa kasi, nguvu na ari mpya ili maisha bora kwa kila Mtanzania yapatikane.

 

Salim Habib, Morogoro

0652 054 343

Baadhi ya madereva hawajui matumizi taa za barabarani

 

“Mara nyingi ninapoendesha gari katika mitaa ya Jiji la Arusha, nalazimika kutumia akili nyingi. Hadi naondoka mjini huwa ninahisi uchovu wa kufanya kazi nzito ya kutumia akili.”

 

Serikali yaahidi kusaidia JKT

Julai 10, mwaka huu, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, aliwaoongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 50 ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Halmashauri ya Geita yatafunwa

* Sh mil 763.8 zakwapuliwa kifisadi

* Mwenyekiti CCM Mkoa ahusishwa

* Waandishi wa habari wapata mgawo

Siku chache baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa za nyaraka zinazoonesha Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilipokea Sh bilioni 11.1 za kununua madawati lakini fedha hizo hazijulikani zilivyotumika, taarifa nyingine zimepatikana zikionesha ubadhirifu wa Sh zaidi ya milioni 763 katika halmashauri.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Hatuwezi kuthibitisha wanaotusaidia

“Tunatambua kuna uwezekano kwamba hao wanaotusaidia wanaweza kuwa na nia tofauti. Hivi ndivyo tunaambiwa na hatuna uthibitisho kwamba haiko hivyo. Lakini tuna ushahidi wa mahitaji yetu na misaada ya vitendo.

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Alizaliwa Aprili 13, 1922 kijijini Butiama, Mara. Alifariki Oktoba 14, 1999 nchini Uingereza.