๐™’๐™–๐™ฃ๐™–๐™ฃ๐™˜๐™๐™ž ๐™ฌ๐™– ๐™‰๐™ฎ๐™–๐™ฌ๐™ž๐™ก๐™ž๐™ข๐™ž๐™ก๐™ฌ๐™– ๐™Ÿ๐™ž๐™ข๐™—๐™ค๐™ฃ๐™ž ๐™‚๐™š๐™ž๐™ฉ๐™– ๐™ฌ๐™–๐™ข๐™š๐™ข๐™ฅ๐™ค๐™ ๐™š๐™– ๐™ ๐™ฌ๐™– ๐™จ๐™๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ฌ๐™š.

๐˜ผ๐™ฉ๐™ค๐™– ๐™จ๐™–๐™ก๐™–๐™ข๐™ช ๐™ฏ๐™– ๐™ช๐™ฅ๐™š๐™ฃ๐™™๐™ค ๐™ฃ๐™– ๐™ช๐™Ÿ๐™ž๐™ค ๐™ฌ๐™– ๐˜ฟ๐™ ๐™ฉ. ๐™Ž๐™–๐™ข๐™ž๐™–.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amewasili na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa Chama na Jumuiya, Viongozi mbalimbali wa Dini na maelfu ya wananchi wa Nyawilimilwa wilayani Geita kwa ujumla wake.

Pamoja na kuwasili kwake, Dkt. Migiro amepata wasaa wa kusalimiana na kuteta kidogo na baadhi ya kundi la watu wenye ulemavu ambapo wamempa salamu zao za shukrani kwa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Rais Dkt. ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ฆ๐˜‚๐—น๐˜‚๐—ต๐˜‚ ๐—›๐—ฎ๐˜€๐˜€๐—ฎ๐—ป kwa namna ambavyo serikali yake anayoiongoza ya awamu ya sita ilivyowagusa walemavu moja kwa moja katika kuwawezesha kiuchumi na kuwawekea mazingira bora na rafiki katika upatikanaji wa huduma za kiafya na kumuahidi kuwa wataendelea kuhamasishina na kushiriki kikamilifu uchaguzi mkuu kwa kwenda kumpigia kura Dkt. Samia, Wabunge na Madiwani wanaotokana na CCM.

Aidha, Dkt. Migiro ametanguliza salamu za ujio wa Dkt. Samia katika kunadi ilani ya CCM (2025/30) Sera na Ahadi zake kwa wananchi hao huku akiwasisitizia wananchi hao kuendelea kuwa na imani na CCM na kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba 29.