Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 16, 2023 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya mazishi ya Marehemu Bernard Membe iliyofanyika kijijini kwake Rondo, Chiponda Mkoani Lindi.

Akizungumza na waombolezaji katika ibada hiyo Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania kumuombea na kuenzi yote mazuri aliyowahi kufanya marehemu Bernard Kamilius Membe wakati wa uhai wake.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Bernard Membe wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Membe yaliyofanyika kijijini kwake, Rondo, Chiponda Mkoani Lindi. Mei 16, 2023 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Bernard Membe wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Membe yaliyofanyika kijijini kwake, Rondo, Chiponda mkoani Lindi. Mei 16, 2023.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Membe yaliyofanyika kijijini kwake, Rondo, Chiponda Mkoani Lindi, Mei 16, 2023 Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na waombolezaji wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Bernard Membe yaliyofanyika kijijini kwake, Rondo, Chiponda Mkoani Lindi. Mei 16, 2023 (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)

By Jamhuri