Mgombea wa Udiwani Kata ya Turwa, Tarime Kupitia CCM Amepita Bila Kupingwa

Mkurugenzi wa Halamshauri ya Mji wa Tarime Elias Ntiruhungwa ameamua kumutangaza aliyekuwa Mgombea udiwani kata ya Turwa kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi Bw Chacha Mwita Ghati kwa madai kuwa amepita bila kupingwa huku akieleza kuwa wagombea Wenzake kutoka vyama vya upinzani wamekosea kujaza fomu jambo ambalo lilisababisha msimamizi Msaidizi wa wa uchaguzi ambaye ni Afisa Mtendaji wa kata kutowateua kuwa wagombea katika Uchaguzi huo mdogo.

Elias amesema kuwa Uteuzi umefanyika na Mgombea wa CCM akawa ameteuliwa pekee yake na baada wagombea wengine kutoka CHAHADEMA, ACT Wazalendo pamoja na NCCR Mageuzi kukosa sifa za kuteuliwa ili waweze kugombea ameweza kupitia mapingamizi yaliyoletwa na wagombea hao baada ya kijiridhisha akiwa na wataalamu wenzake akaamua kutangaza Mgombea huyo Mmoja kuwa amepitwa bila kupangwa.

“Hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 45 kifungu kidogo cha pili cha sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa No4 ya Mwaka 1979 sura ya 292 kinasema endapo mgombea aliyeteuliwa ni mmoja baada ya pingamizi kukamilishwa.

Msimamizi wa uchaguzi ambaye ni mimi anapaswa kutalifu mgombea kwa barua kuwa amepita bila kupingwa na pia nitafaamisha tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhusu suala hilo, hivyo mimi kama Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Tarime Mjii natangaza rasmi kuwa Mgombea wa CCM Chacha Mwita Ghati amepita bila kupingwa” alisema Elias.

Pia Mkurugenzi huyo amemutaka Chacha kusubiri mpaka pale atakapoapishwa na kukabidhiwa cheti kutokana na tarehe za uchaguzi zilizotangangazwa na Tume ya Taifa ya Uchgaguzi.“Pamoja na kwamba amepita bila kupingwa asianze kazi ya udiwani kwa sababu tarehe za Uchaguzi hazijafika mpaka Agosti 12 Mwaka huu na sisi ndo tutaapisha diwani huyo na kuanza kazi ya udiwani lakini kama kuna mtu upande wa pili hajakubaliana na maamuzi yangu sheria iko wazi atakata rufaa” alisema Ntiruhungwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tarime Mkoani Mara Elias Ntiruhungwa akitanganza rasmi mgombea Udiwani kata ya Turwa Chacha Mwita Ghati CCM baada ya kupita bila kupingwa.

Wananchi wakiwa katika ofisi ya Kata ya Turwa kwa ajili ya kusikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime akitangaza rasmi Mgombea udiwani kata ya Turwa.

Baadhi ya wanachama wa CCM Wakiwa na mgombea udiwani kata ya Turwa Chacha Mwita Ghati wa pili kutoka kushoto aliyevaa sare ya chama hicho.