JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mheshimiwa Sitta acha kututania!

Wiki iliyopita zilichapishwa habari nyingi, ila nimejikuta na shindwa kujizuia nashawishika kuandika jambo juu ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mheshimiwa sana, Samuel Sitta, ‘Mzee wa Kasi na Viwango.’ Mheshimiwa huyu ametoa kauli kuwa Bunge Maalum la Katiba lazima liendelee na kura zipigwe.

TMF yatoa ruzuku kwa vyombo vya habari 16

Mfuko wa vyombo vya habari nchini (TMF), kwa mara nyingine, umetoa ruzuku ya Sh. bilion 1.7 kwa vyombo vya habari 16.

Posho EAC kufuru

*Kila kikao mbunge analipwa Sh laki 9

 

Posho ya Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) ni Sh. 940,000 kwa siku. Malipo hayo ni kwa kila mbunge hata kama hakudhuria vikao vya Bunge.

Kutokana na utoro wa wabunge ambao umefikia kiwango cha kukwamisha vikao, juhudi za chini kwa chini zimeanza kufanywa na baadhi ya wabunge ili kubadili kanuni.

Mmoja wa wabunge hao ameiambia JAMHURI kuwa juhudi hizo ni pamoja na kuhakikisha kuwa mbunge ambaye hahudhurii kikao, anakosa posho.

ISIL yazidi kuitesa Marekani, Waarabu nao waingilia kati

WAPIGANAJI wa kundi la Taifa la Kiislamu la Iraq na Levant (ISIL), wanazidi kuwatesa Wamarekani, kiasi kwamba hata Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA), limekiri kwamba mapambano dhidi ya waislamu hao ni magumu.

Paroko RC aishiwa uvumilivu, awacharaza viboko Wasabato

 

PAROKO wa Parokia ya Urumi, iliyoko Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, Padri Peter Twamba, amewajia juu waamini wa Kanisa la Waadivetisti Wasabato, waliotuhumiwa kukashifu imani ya Kanisa Katoliki (RC).

Tukio hilo lilitokea kanisani hapo, Jumapili ya 23 ya mwaka ‘A’ (kijani) ya Septemba 7, mwaka huu saa 3 asubuhi mara baada ya misa ya asubuhi kanisani hapo.

Nyalandu aanza kulipa ndege aliyofadhiliwa

Mara baada ya Balozi Khamis Kagasheki kujiuzulu kutokana na shinikizo la wabunge kadhaa, baada ya taarifa ya James Lembeli juu ya Operesheni Tokomeza kuwasilishwa bungeni Novemba, mwaka jana; Lazaro Nyalandu, wakati huo akiwa ni Naibu Waziri katika Wizara ya Maliasili na Utalii, alisafiri sana huku na kule nchini.