JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Madai ya Nyalandu na majibu ya hoja zake

Katika gazeti la Jamhuri la Jumanne Agosti 19 – 25, 2014 ISSN No. 1821-8156 Toleo No. 150, zilichapishwa taarifa potofu zenye  kichwa cha habari;

KASHFA IKULU;

·    Nyalandu atumia Leseni ya Rais kuua wanyamapori 704 bure,

·    Watakaouawa wamo pia tembo 8, chui 8, Simba 8, ndege,

·    Wauaji ni Wamarekani marafiki wa Waziri wa Maliasili.

Mafanikio yana gharama!

David O. Oyedepo anatajwa kuwa ndiye mchungaji tajiri kuliko wote duniani. Ndiye mwanzilishi wa Kanisa la Winners Chapel International, kanisa ambalo linatajwa kumiliki jengo la kanisa kubwa kuliko yote duniani, likiingiza watu 50,400 kwa mara moja. Jengo hili Ota nje kidogo ya jiji la Lagos la Nigeria na ndiyo Makao Makuu ya Kanisa hilo duniani.

Yah: Ningependa Rais ajaye afanye yafuatayo?

Wiki jana niliandika barua kama hii nikisema huyu ndiye mwenye sifa za kuwa Rais wa awamu ya tano, niliainisha sifa chache kutokana na ujinga wangu, sifa ambazo baadhi ya watu wanaweza kusema kwa utaratibu wa maisha ya sasa ya utandawazi siyo rahisi kumpata kiongozi mwenye sifa hizo.

Ujana, uzee sio sifa za kuwa Rais wa Tanzania

Ni Kitambo sasa, Watanzania wamo katika fikra na harakati za kumpata Rais mpya hapo mwakani, kwa kipindi cha miaka mitano ijayo baada ya Rais wa sasa Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kukamilisha muda wake wa uongozi na utawala wa miaka kumi.

Huduma mbovu za jamii zitaangusha CCM

Tunapozungumzia huduma za jamii huwa tunazungumzia masuala ya elimu, afya ,maji, umeme, huduma kwa wazee, huduma kwa walemavu na kadhalika.

Majibu kwa porojo za Nyalandu

Asoma na kujibu kiubabaishaji tuhuma kwenye magazeti aliyodai awali kuwa ni ya kufungia maandazi. Kwa muda mrefu sasa baadhi ya magazeti hapa nchini yamekuwa yakiujuza umma ukweli kuhusu Lazaro Nyalandu, ambaye kwa takriban miezi tisa sasa ni Waziri wa Maliasili na Utalii. Habari kumhusu Nyalandu zilianza kutolewa hata kabla hajawa Naibu Waziri wa Wizara hiyo, wakati angali Naibu Waziri katika Wizara ya Viwanda na Biashara, chini ya Cyril Chami wakati huo. Katibu Mkuu wa Wizara hiyo wakati huo alikuwa Joyce Mapunjo.