JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Zitto amuumbua Spika

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Spika Anne Makinda, asipodhibitiwa, ataiua nchini kutokana na uongozi wake wa kiimla.

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Viongozi wabovu hulizwa na matatizo

“Viongozi wabovu wenye mioyo ya kuku, hulizwa na matatizo; bali watu madhubuti, wenye mioyo thabiti, hukomazwa nayo… hatima ya nchi yetu ni jukumu letu. Kwa pamoja tunaweza kuisaidia nchi yetu kusonga mbele kuelekea kwenye haki zaidi na usawa zaidi kwa Watanzania wote.”


Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA

Jumamosi Februari 9, 2013 Mtibwa Sugar Vs Azam FC Toto Africans Vs Coastal Union Kagera Sugar Vs Mgambo JKT TZ Prisons Vs African Lyon JKT Oljoro Vs Simba SC

Mambo muhimu Stars kucheza AFCON

Kocha wa timu ya soka ya taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen, amesema kuwa haoni sababu itakayoizuia Tanzania kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2015.

Ligi Kuu Bara isiwe ya Simba, Yanga

Mara nyingi ubingwa wa mashindano ya soka ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, umekuwa ukibebwa na Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya jijini na Dar es Salaam Young Africans (Yanga), yenye makao yake mitaa ya Jangwani na Twiga, kana kwamba timu nyingine hazina wachezaji mahiri wenye uwezo wa kushinda.

Yah: Jamani kama ningelikuwa mbunge

Wanangu mu hali gani, siku zote nawaandikia barua lakini siwaulizi hali zenu, mara zote huwaeleza siha yangu bila kujua siha zenu. Nimeona sitendi haki kwa kuwa kujua hali zenu ni jambo bora zaidi kuliko kuwafikishia ujumbe wangu, maana naweza kuwa nafikisha ujumbe katika uwanja wa makaburi ambako mmelazwa kutokana na ugumu wa maisha.