JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ushindi wa Uhuru Kenyatta ulivyopokewa Kenya

Wafuasi wa Uhuru Kenyatta walijitokeza mwishoni mwa wiki kusherehekea ushindi wake wa kiti cha urais wa Kenya. Uhuru amepata ushindi kwa asilimia 50.03 dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Raila Odinga.

Chinja chinja ya Polisi yatikisa Geita

*Mfanyabiashara auawa, wampora dhahabu, mamilioni

*Mtoto, mke, majirani waeleza ‘sinema’ yote ilivyokuwa

Lukumani Yunge (13) ambaye ni mtoto wa Yemuga Fugungu (31) aliyeuawa wiki moja iliyopita nyumbani kwake katika Kitongoji cha Masota, Kata ya Uyovu Lunzewe wilayani Bukombe, ameeleza namna polisi walivyomlazimisha awaonesha chumba kinachotumiwa na baba yake kuhifadhia dhahabu.

Siri za nyumba za mawaziri zavuja

*Baadhi wadaiwa ‘kuzikacha’

Matumizi ya nyumba za mawaziri jijini Dar es Salaam yamegubikwa na siri nzito. Inadaiwa kuwa baadhi ‘wamezitosa’ kwa kisingizio cha kukosa usiri.

Lowassa amponza Kibanda

 

*Taarifa za awali zahusisha kutekwa na urais 2015

*Risasi aliyopigwa ilifumua jicho, ikatokea kisogoni

Tukio la Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, kutekwa, kupigwa, kung’olewa meno, kukatwa kidole na kung’olewa kucha limeanza kuhusishwa na mlengo wa kisiasa.

NUKUU ZA WIKI 68

Nyerere: Tunamtaka rais anayechukia rushwa

“Rushwa ni adui wa haki. Tunamtaka rais atakayelitambua hilo, atakayeichukia rushwa hata ukimuangalia aoneshe kweli anaichukia rushwa, sio rais anayesema kweli rushwa ni adui wa haki…. lakini ukimwangalia usoni unashangaa na kusema…. aaaah kweli huyu?”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Leo ni leo Man United vs Real Madrid

Leo ni leo, asemaye kesho ni mwongo. Timu maarufu za soka barani Ulaya, Manchester United na Real Madrid, leo zinatinga uwanjani kumenyena katika kinyang’anyiro cha Mabingwa wa Ulaya (UEFA). Manchester United inatinga katika mtanange huo ikiwa inajivunia mshambuliaji wake, Christiano…