Latest Posts
Hofu yatanda Katiba mpya
*Ananilea: Rais akipenda ataokoa jahazi Wingu zito limetanda juu ya mchakato wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya viongozi wa dini na wanaharakati kutabiri kifo chake. Baadhi wamekosoa mfumo wa Bunge Maalum la Katiba, na…
Vibwanga vya Waziri Lazaro Nyalandu
*Madudu yake yanamchafua Rais Kikwete
Mara tu baada ya mawaziri wanne kujiuzulu na wengine kuondolewa kutokana na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu katika Operesheni Tokomeza, mwandishi mmoja aliandika makala iliyokuwa inasomeka, “Kikwete ana mkosi gani na mawaziri wake?”
TCAA nako kwafukuta ufisadi
*Wakurugenzi wahariri Waraka wa Hazina
*Mbinu hiyo yawafanya walipane mamilioni
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), inakabiliwa na tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Fadhil Manongi, hadi wiki iliyopita bado alikuwa akiendelea na dhima za kiofisi licha ya muda wake wa kung’atuka kuwadia.
Wakati Manongi akijiandaa kuiacha ofisi hiyo, kumekuwa na malalamiko ya matumizi mabaya ya fedha miongoni mwa wakurugenzi ambao ni washirika wake.
Siku za Kipande bandarini zahesabika
*Ni baada ya kuthibitika anatumia vibaya jina la Rais Kikwete, Ikulu
*Amuagiza Mwakyembe amchunguze, wafuatilia kumtukana Balozi
* Mtawa, Gurumo nao wakana, Mwakyembe adaiwa kumwogopa
*Aendelea kukaidi maagizo ya Bodi, amng’oa rasmi aliyeomba kazi yake
Na Deodatus Balile
Siku za Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mzee Madeni Kipande (58), kuendelea kuwa madarakani zinazidi kuyoyoma baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na tabia yake ya kutumia jina la Rais kuhalalisha matendo yake yenye kukiuka sheria za utumishi wa umma.
Habari za uhakika kutoka Ikulu na kwa baadhi ya mawaziri waandamizi, zinasema Rais Kikwete baada ya kupata taarifa za Kipande kutumia vibaya jina lake, alichukia na kuamua kumwita Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, na kumpa maagizo mazito.
Vituko vya DC Geita
Na Victor Bariety, Geita
Sehemu ya kwanza ya makala hii ilielezea vituko vinavyofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Omari Manzie Mangochie, vikiwamo vya kuzuia ujenzi wa mnara wa simu za mkononi na kutangaza vita na waandishi wa habari. Sasa endelea na sehemu hii ya pili.
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Omari Manzie Mangochie ambaye anatajwa kama kiongozi anayezalisha migogoro na kukwamisha shughuli za maendeleo wilayani hapa. Anatuhumiwa pia kumng’oa Mwenyekiti wa Chama chake cha Mapinduzi (CCM) wa kijiji cha Mnyara, hivyo kuwapatia wapinzani mwanya wa uongozi.
Katika tuki hilo la aina yake, Mangochie baada ya kumvua uongozi Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyara, Makoye Roboyanke, aliitisha uchaguzi mdogo na kuwaamuru wananchi kupiga kula za wazi mgongoni mwa wagombea kinyume cha taratibu za uchaguzi.
Kitendo hicho kilizua tafrani kubwa kwani pamoja na wananchi kukubali matakwa ya Mkuu huyo wa wilaya kwa kuwachagua viongozi wao nyuma ya migongo, CCM kilichokuwa kimeweka mizizi eneo hilo kilibwagwa na kusababisha msimamizi wa uchaguzi kukimbia na matokeo ili kujinusuru na kipigo kutoka kwa wananchi hao.
Inadaiwa kuwa uamuzi huo wa Mangochie wa kumvua uongozi kada huyo wa CCM bila kufuata utaratibu umesababisha wananchi wa eneo hilo kukihama chama hicho tawala na kujiunga na vyama vya upinzani ambavyo hapo awali havikuwa na nguvu kwenye kijiji hicho ambapo wameiomba Serikali kuingilia kati mgogoro huo.
Akizungumza na JAMHURI kijijini hapo hivi karibuni, mwenyekiti huyo wa kijiji alisema uamuzi huo wa Mangochie umemdhalilisha na umeonesha ni jinsi gani asivyoheshimu vikao halali vya CCM.
Anahitajika Sokoine mwingine 2015
Mengi mazuri yanayomhusu Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine, yamesemwa na yanaendelea kusemwa.
Kwa Mtanzania yeyote wa kweli, kamwe hatachoka kusikia mengi yaliyofanywa na Sokoine wakati wa uongozi wake.
Miaka 30 sasa tangu alipoaga dunia, shujaa huyu hajulikani kwa vijana wengi wa Tanzania. Safu hii ni fupi mno, kiasi kwamba haiwezi kumweleza japo kwa nukta mtu huyu hata akaeleweka kwa vijana wengi.
Itoshe tu kuwaasa vijana kuyasaka kwa udi na uvumba maandiko yanayomhusu shujaa huyu wa Tanzania, ambaye mfano wake kwenye nafasi ya Waziri Mkuu, haujapatikana.
Licha ya wengi kumzungumza Sokoine, hiyo haitoshi kutufanya nasi tusiweke neno wakati huu wa kumkumbuka.
Moringe alikuwa kipenzi cha Watanzania wengi, hasa makabwela. Alipendwa na watu wa jinsi, hali na rika zote. Hakuwa na makuu. Alikuwa mcha Mungu wa kweli. Hakuwa kiongozi wa kupayuka-payuka, bali alikuwa mpole, msikivu na mwenye kusimama katika ukweli na haki. Uwajibikaji na uadilifu ndiyo uliokuwa msingi mkuu wa Sokoine.