JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

FIKRA YA HEKIMA

Wawekezaji wazawa waungwe mkono

Watanzania tumejenga kasumba mbaya ya kuwathamini wawekezaji wa kigeni. Wakati huo huo tumekuwa kikwazo kwa wawekezaji wazawa!

Wabunge wa CCM wameshindwa kazi?

Sina sababu yoyote ya kuwavunjia heshima wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Lakini katika enzi hizi za ukweli na uwazi sioni, sababu ya kusita kuzungumzia masuala nyeti kwa ukweli na uwazi. Lengo langu ni kuwaomba waone ugumu wa uchaguzi wa mwaka 2015.

Kashfa zimelilemea Jeshi la Polisi

Wakati fulani wabunge waligombana na aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Omar Mahita. Hoja ilikuwa kwamba Jeshi la Polisi lilistahili kuvunjwa ili liundwe upya. Wakatoa mfano wa Jeshi la kikoloni la King African Rifles (KAR), lilivyovunjwa baada ya maasi ya mwaka 1964 na kuundwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Wachochezi wa vurugu waadabishwe ipasavyo

Wiki iliyopita, Jeshi la Polisi lilitangaza kumtia mbaroni mtu anayedaiwa kuwa kinara wa kusambaza ujumbe wa kuchochea chuki na uhasama hapa nchini, kupitia simu za kiganjani.

Stars tupeni raha Watanzania

Timu ya Soka ya Taifa (Taifa Stars) inatarajiwa kushuka dimbani Juni 8 mwaka huu, kucheza na Morocco katika mchezo wa kuwania kufuzu kushiriki Mashindano ya Kombe la Dunia 2014 yatakayopigwa nchini Brazil.

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Chama kisilazimishe watu kukichangia fedha

“Kwamwe chama [cha siasa] kisitoze kodi, au ushuru, au malipo ya nguvu-nguvu kwa mtu yeyote, awe mwanachama au si mwanachama. Michango yoyote ya fedha inayotolewa kwa ajili ya shughuli za chama lazima itokane na ridhaa ya mtoaji mwenyewe.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.