Latest Posts
Serikali ni mtuhumiwa pekee kipigo cha Dk. Ulimboka
Mkononi nina Gazeti la JAMHURI (Julai 10-16, 2012) toleo Na. 33. Nimevutiwa na kichwa cha habari, ‘Dk. Ulimboka siri zavuja’. Nimevutiwa na habari hii kwa sababu ni moja ya mambo yanayoigusa jamii kwa sasa ikizingatiwa kuwa bado hali yake kwa walio wengi hatuijui, lakini pia mgomo wa madaktari bado unaendelea (naomba mgomo huo uishe ili tuweze kupata huduma).
Siri ya mafanikio yangu kiuchumi
Sasa nimeamini kuwa ‘la kuteleza haliwezi kutembea’ na ‘la kuvunda halina ubani’. Wiki mbili zilizopita niliandika makala yaliyokuwa na kichwa chahabari, ‘Je, machozi ya walimu yatamimina fedha mitaani?’
Mchechu: Tanzania si masikini
“Maelezo kwamba Tanzania ni nchi masikini yananikera. Imefika mahala wanasiasa wanadhani ili uwe kiongozi bora ni lazima ujiainishe kuwa unatatea masikini. Natamani tukose misaada kwa miaka mitano, tutapata akili na kutumia vyema utajiri tulionao. Hatustahili misaada kabisa maana nchi hii inao utajiri wa kutosha.”
Maneno haya ameyasema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, akiwaambia wahariri wa vyombo vya habari mjini Morogoro kuwa mawazo ya Watanzania yanapaswa kufikiria kufanya kazi zaidi badala ya kutegeshea misaada.
Uncle Tom naye atafukuzwa Yanga kama Timbe au Papic?
Msimu uliopita, Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake mitaa ya Twiga na Jangwani jijini iliyokuwa ikitetea ubingwa wake, ilifundishwa na makocha watatu kwa nyakati tofauti. Kwanza ilianza ligi hiyo, Agosti mwaka jana ikiwa na Sam Timbe, Mganda…
Tuache kasumba ya kupuuza kila linalozungumzwa na Wapinzani
Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu, amezungumza mambo mazito mno mwishoni mwa wiki. Sehemu ya hotuba yake tumeishapisha neno kwa neno ndani ya gazeti hili.
Ufisadi watikisa Bunge
*Unahusu kada wa CCM anayechimba urani
*Profesa Tibaijuka amtwika mzigo Jaji Werema
*Naibu Spika aagiza Waziri Muhongo ajiandae
*Sinema nzima imeibuliwa na Halima Mdee
Wafanyabiashara ndugu wanaodaiwa kubadili matumizi ya ardhi kutoka uwindaji wa kitalii na kuanza harakati za uchimbaji madini ya urani, wameibua mgongano mkubwa bungeni na serikalini. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amemwomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, asaidie kupata utatuzi kashfa hiyo.