Rais Mwinyi ahutubia Siku ya Wafanyakazi Duniani viwanja vya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika viwanja vya mpira Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa ajili ya kupokea Maandamano ya Wafanyakazi kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi,  yaliyofanyika katika Mkoa wa Kaskazini Unguja leo1-5-2023 na (kulia kwa kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga.(Picha na Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akipokea maandamano ya Wafanyakazi Kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi yaliyofanyika katika viwanja vya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja leo Mei 1, 2023.(Picha na Ikulu)