Simba yang’ara ugenini Ligi Mabingwa Afrika

Simba SC wameng’ara ugenini baada ya kuwachapa wenyeji Big Bullets bao 2-0 mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika inayopigwa kwenye uwanja wa Taifa Bingu, Malawi.

Moses Phiri aliiandika bao la kwanza Simba mnamo dakika ya 29 na mnamo dakika ya 83 John Bocco aliiandikia timu yake bao la pili.

Timu hizo zitarudiana Septemba 17,mwaka huu katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.