Wahamiaji haramu na walowezi wanaoishi hapa nchini wanatumia mwanya wa usajili wa laini za simu wa ‘mwendokasi’ kujipatia vitambulisho vya taifa, JAMHURI limebaini. 

Hali hiyo imeelezwa kuwapo katika mikoa ya pembezoni mwa nchi, na tayari malalamiko kadhaa yamekwisha kupelekwa kwenye mamlaka husika. Miongoni mwa maeneo yanayotajwa kukumbwa na hali hiyo ni wilaya za Longido na Ngorongoro.

“Sisi hapa Ngorongoro hali hiyo ipo kwa sababu hata wale waliokuwa blacklisted wakazuiwa kupewa vitambulisho vya mpiga kura, sasa wamepewa vitambulisho vya taifa,” kinasema chanzo chetu.

Imeelezwa kuwa hata viongozi waandamizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika ngazi ya wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro ambao walinyimwa haki za uraia kwa vile ni walowezi kutoka nchi jirani, baadhi yao wamepata vitambulisho kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Hali hiyo imemfanya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, acharuke na kutoa maagizo kwa wahusika.

Akizungumza na JAMHURI, Lugola anasema: “Najua wapo wanaotumia fursa hii ya msongamano wa kusajili laini za simu kwa ajili ya kupata vitambulisho vya uraia. Nawaonya waache mara moja.

“Wanaona watu tuna presha ya kusajili laini wao wanapenya, ninatoa mwito kwa wananchi wote kuwa macho. Ulinzi wa taifa letu ni wa vyombo vya ulinzi na usalama na wananchi wote wenye mapenzi mema.

“Natoa rai kwa kila mwananchi kuwa makini kwa kutoa taarifa kwenye vyombo husika pale wanapoona au wanapoambiwa kuna mtu au watu wasiokuwa raia wanaopenya na kupata ‘uraia’ kwa njia za mkato.

“Kila mwananchi asisite kutoa taarifa ya maandishi, ya mdomo au kuweka pingamizi kwa mhamiaji haramu yeyote anayepata kitambulisho cha taifa. Wenye taarifa za watu hao wanaweza kutuletea kwa njia ya siri na sisi tutahifadhi siri hizo na wala majina yao hayatatangazwa au kujulikana,” anasema.

Waziri Lugola anasema ni rahisi zaidi kwa wananchi kuwabaini wahamiaji haramu wanaojipatia uraia kwa kuwa wanaishi nao.

“Wananchi wanakaa nao, wanawajua. Kila Mtanzania awe na uchungu na nchi yetu, maana bila hivyo tunaweza kujikuta tunakuwa na wageni wengi wanaojipatia uraia kwa njia haramu,” anasema.

Kuhusu ukubwa wa tatizo hilo mkoani Arusha, hasa katika maeneo ya Longido na Ngorongoro, Waziri Lugola anasema: “Maeneo ya pembezoni yana changamoto nyingi, na hilo la baadhi ya wageni kuja nchini na kuwa viongozi, naamini Uhamiaji watalishughulikia kwa mujibu wa sheria.”

Katika hatua nyingine, waziri huyo anasema kazi ya utoaji vitambulisho na uandikishaji wa laini za simu inayoendelea hailengi kuwakomoa wananchi, bali inalenga kuleta tija zaidi kwa nchi na wananchi.

“Hakuna nchi inataka kuwaumiza au kuwakomoa wananchi wake, huu ni mfumo mzuri sana wa usalama wa watu na nchi yetu. Wananchi wasichukulie kuwa hii ni kero. Usajili wa laini za simu pamoja na vitambulisho vya NIDA vitasaidia mambo mengi sana kwenye usalama na kichumi. Tutajua nani ni nani, yuko wapi na anafanya nini. Wahalifu watabanwa vizuri zaidi na kero nyingine kama za kudaiwa barua za watendaji zitapungua kwa kuwa na kitambulisho cha NIDA. Wananchi wasione kuwa serikali inawakomoa. Kama laini imefungwa ni kwa muda tu na baada ya usajili mwananchi anaweza kurejesha laini yake ile ile au akiamua anapata nyingine,” anasema Lugola.

Mmoja wa viongozi waandamizi wa Idara ya Uhamiaji mkoani Arusha amezungumza na JAMHURI na kueleza kuwa pamoja na changamoto za usajili wa laini za simu, wamejitahidi kuhakikisha hakuna mlowezi au mhamiaji haramu anayepata kitambulisho cha uraia cha NIDA.

Akizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina, anasema: “Kweli Ngorongoro kuna rejesta ya wahamiaji haramu na walowezi. Nadhani idadi ni kama 250 hivi, hao wanajulikana na kwa kweli tumehakikisha hawapati vitambulisho vya uraia. Majina yao yameingizwa kwenye system (mfumo) kiasi kwamba jina likionekana tu tunapata taarifa.

“Fomu zote za maombi ya vitambulisho tunazipitia na sharti zisainiwe, na kila anayeandikishwa tunapitia taarifa zake na kuzipitia kwa mtu mmoja baada ya mwingine – kwa hiyo nikuhakikishie kuwa kama yupo aliyepenya, tutampata,” anasema.

Ofisi hiyo ya Uhamiaji Mkoa inasema miongoni mwa wanaochunguzwa uraia wao ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ngorongoro, Ndilango Senge. 

Katika Kijiji cha Ololosokwan, Tarafa ya Loliondo, Ngorongoro, raia wa Kenya, Esophio Parmwat; licha ya kubainika kuwa si raia wa Tanzania, aliwania uenyekiti wa serikali ya kijiji hicho.

Idara ya Uhamiaji Wilaya ya Ngorongoro katika barua yake kwenda kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, ilisema kuwa Parmwat si raia wa Tanzania, na kwa sababu hiyo hapaswi kuwania nafasi yoyote ya uongozi.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ngorongoro, Roza Kiromo, licha ya kushika wadhifa huo, yuko kwenye orodha ya watu ambao uraia wao una shaka.

Orodha ya walowezi wanaoishi Loliondo

Katika vijiji kadhaa katika Tarafa ya Loliondo kumepatikana majina 224 ya ‘Wakenya’ ambao, ama ni wahamiaji haramu, au walowezi. Wanaishi na kuendesha shughuli zao huku wakipata haki zote kama Watanzania.

Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa miongoni mwa walowezi hao ambao uraia wao unatiliwa shaka, tayari wamekwisha kupata vitambulisho vya NIDA kama raia halali, na si walowezi. Hali hiyo inakinzana na taarifa ya Uhamiaji Mkoa wa Arusha. Ifuatayo ni orodha iliyoandaliwa miaka kadhaa iliyopita:

1: Peter Kiromo

2: Elizabeth Nairushiye

3: Kennedy Manyeki

4: Katikasha Kamanga

5: Risa Kamanga

6: Huho Daniel

7: Jackson Manyeki

8: Glady Kurgat

9: Elizabeth Ongetont

10: James Koromo

11: John Nzuna

12: Anna Ramasigonde

13: Omaria Lengaaki

14: Nangaya Lengaaki

15: Ndito Lengaaki

16: Kalee Saitabau

17: Najara Koleli

18: Joshua Saitabau

19: Timan Rika Yion

20: Ngopeesho Olekorkai

21: Ngisu Olenanyokie

22: Joel Siyianga

23: Sikemboi Sisi

24: Noosokono Koleli

25: Lasaru Saitabau

26: Noorkorea Sisi

27: Olemeen Ngoikor

28: Joel Lengaaki

29: Elija ole Matian

30: Joel Siyanka

31: Parkipoi Murera

32: Iman Olemetian

33: Nangida Olemen

34: Joshua Mwarabu

35: Oloibor Ngapai

36: Andrew Nkanuma

37: Sintako Nkanuma

38: Ngaina Saitabau

39: Nosilat Naingisa

40: Susana Massago (mama)

41: Binifas Massago

42: Oloongoshoka Ndaiya

43: Lengoko Saitabau

44: Modolu Yengo

45: Sirere Mpoe

46: Oleengot Engo

47: Oletimoi Stephen

48: Joshua Marabui

49: David Sais

50: Lekakiuy Sananka

51: James Massago

52: Bebi Massago

53: John Ngile

54: Ole Kileu

55: Ole Sasii

56: Joel Karori

57: Chuma Shambarao

58: Olooseenge Rea

59: Sakaria Narikai

60: Orandaya Kitipa

61: Alex David

62: Dopoi Kitipa

63: Kosia David

64: Porosooi Ndaiya

65: Boma ya Oleshung

66: Boma ya ole Serei-Kututuo

67: Boma ya Olekitipa

68: Nganuma Lemorara

69: Nganeni Lemorara

70: Ng’onene Nkanuma

71: Anna Gathu

72: Ruth Kabulunze Musomba

73: David Marko Sessat

74: Naomi Marko Sessat

75: Josephine Kuria

76: Joseph Kabulunze Musomba

77: Elizabeth Musumba

78: Marco Muhinge

79: Christine Musomba

80: Ndolee Temwee

81: Jane Koromo

82: Philipo Justus Marco

83: Pareyo Kitipa

84: Olengutie Saing’eu

85: Lekinyit Reyia

86: Esophie Parmat na ndugu zake

87: Kararit Ndaiya

88: Peter Kashal

89: Olemundere

90: Kisarunga Leitura

91: Luthia Ngelenche

92: Christine Francis William

93: Christopher Marco Sessat

94: Denis Okirigiti

95: Aizack Tura

96: Magreth Kiromo

97: Peter Robert Kiromo

98: Steven Kabulunje (dereva Hifadhini)

99: Peter Mtune Kaput

100: John ole Keroto

101: Siminde Lonyori

102: Anna Ngelenche

103: Zakayo Sesat

104: Pius Mtune Kaput

105: Emmanuel Samwel

106: Joseph Sessat

107: Estomih Manyeki

108: Joachim Manyeki

109: Felomona Mtune Kaput

110: Godfrey Kiromo

111: Godwin Mtune Kaput (Mwalimu Halmashauri)

112: Lazaro Sessat

113: Beatrice Kimoro

114: Evaline Bilechi

115: Saimon Sessat

116: Emmanuel Sassat

117: Lucy Chambii

118: George Mtune Kaput

119: Yasinta Dunya

120: Anna Cheburge

121: Joyce Marko

122: Elizabeth Robert

123: Mamiam Koira

124: Lilian John

125: Josephine Koillah

126: Sananga Cooss

127: William Sangupa

128: Coos

129: Olekoreko

130: Amos Olekoreko

131: Joseph Olekoreko

132: Joseph Sessat

133: Mery Kuyato

134: Joseph Kipkia

135: Gudito Nyange

136: Marco William Mabwa

137: Yeremia Olekoreko

138: Napirura Olengopiri

139: Mapena Olengopiri

140: Manina Olenanyika

141: Kiparian Manina

142: Emmanuel Mtune Kaput

143: Nayeilo Angangi

144: Ndina Manina

145: Moris Manina

146: Soinkei Olekumbe

147: Naaramataki Olekumbe

148: Saaloi Leshashi

149: Langoi Leshashi

150: Sabina James Kiromo

151: Rozi Kiromo

152: Lourence Kiromo

153: Emmanuel Kiromo

154: Ateiti Sumare

155: Orkedienye Kapiro

156: Saruni Ngurumwa

157: Sanare Koshara

158: Kisoku Karbolu

159: Memus Sadira

160: Nanjiko Shukur

161: Kipuri Karbolo

162: Nginandei Melejeki

163: Makoi Melejeki

164: Kanaya Karbolo

165: Napatao Meyane

166: Maripet Purengei

167: Oloishuro Kariro

168: Oleshololoi

169: Kingorosh Manatiny

170: Frank Mtune Kaput

171: Kanai Mbatiany

172: Kashing Pikoyan

173: Naingei Koikay

174: Simore Letuluko

175: Nareyo Olekandika

176: Oleniboo

177: Michael Kitipa

178: Kayo Kitipa

179: Korema Mako

180: Shukuru

181: Olonyikid Sironike

182: Olokose Kapiro

183: Karungu

184: Moriko Ngurumwa

185: Shinga Mboe

186: Olorupa Pere

187: Sangau Mbatiany

188: Kararinyayia

189: Olesironik

190: Molinge Oloso

191: Orkelese Ndaiya

192: Ntumaini Nkanuma

193: Nteetu Nkanuma

194: Kosiando Tuke

195: Sopiya Kosiando

196: Daudi Mtune Kaput

197: Juliana Mtune Kaput

198: Francis Mabwa

199: Yohana Sessat

200: Saitoti Kosiando

201: Tina Leshana

202: Shirimu Kuya

203: Ndooriti Koleli

204: Ngicha Oleneko

205: Musu Ngicha

206: Lonyokie Ngicha

207: Tiene Ngicha

208: Titio Ngicha

209: John Kamanga

210: Mbizi Ololeng’a

211: Olengaiki Olepombo

212: Joseph Siere

213: Melejeki Olemunya

214: Saitoti Ngekee

215: Lesidai Melejeki

216: Koika Melejeki

217: Mbaayi Kosiando

218: Ndima Kosiando

219: Koleli Lesite

220: John Koleli

221: Kijooli Melejeki

222: Esophip Parmwat

223: Marco Parmwat

224: Kunday Parmwat

By Jamhuri