YANGA YAFUNGA MWAKA KWA KIPIGO CHA 2-0 KUTOKA KWA MBAO FC

Yanga leo imefunga mwaka vibaya kwa kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Mbao fc ya mwanza,
mabao yote ya mbao yamefungwa na Habib Aji kwenye dakika ka 52 na 70.
kutokana na mchezo huo sasa unaiondoa yanga kwenye orodha ya timu zisizofungwa kwenye mechi zote za Ligi kuu, Sasa zimebaki timu mbili pekee Simba na Azam ambazo mpaka sasa hazikufungwa katika michezo yao waliyocheza ya Ligi Kuu.
Yanga imebakia na point 21 na wameshacheza mechi 12, wapo kwenye nafsi ya tatu mbele ya Azam na Simba ambazo zote zina point 26 zikiwa zote zimeshacheza michezo 12.