Polisi jijini Nairobi wamesema watu 23 wamefariki dunia kufikia sasa,huku uharibifu wa mali, kufungwa kwa baadhi ya barabara pamoja na wakazi wengi kulazimika kuhama makazi yao kutokana na hali hiyo.
Aidha zoezi la uokoaji bado linaendelea kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku kucha na kusababisha mafuriko makubwa katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo.
Taarifa ya polisi inaeleza kwamba watu 29 waliokolewa kutoka maeneo mbalimbali na kwa sasa wanapokea msaada unaohitajika.
Vikosi vya uokoaji bado vimeendelea kuwepo katika maeneo yaliyoathirika zikijibu simu za dharura na kuendeleza operesheni za utafutaji na uokoaji.
Mamlaka zinaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu ili kuhakikisha usalama na ustawi wa wananchi , wakazi na raia wa kigeni.



