DP World imetoa msaada wa gari la wagonjwa kwa Idara ya Zimamoto na Usalama ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Bandari ya Dar es Salaam.

Ambulance hiyo itasaidia kuimarisha huduma za dharura za matibabu ndani ya bandari na kuwahudumia wadau wote wa bandari, wakiwemo wafanyakazi na wakandarasi wa DP World, wafanyakazi wa bandari, mabaharia pamoja na wageni.

Mpango huu ni dhamira endelevu ya DP World katika kuimarisha afya na usalama, uimara wa shughuli za kiutendaji, pamoja na ustawi wa jamii ya bandari.