Hongera Nassari, hongera Chadema
Wapigakura wa Arumeru Mashariki wameamua. Wamemchagua mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joshua Nassari kuwa mbunge wao. Nassari amewashinda wagombea wengine saba wa vyama vya siasa, akiwamo Sioi Sumari aliyekuwa akiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM).