Na Mwandishi Wetu,JamhuriMedia,Mara

MgodiI wa dhahabu wa Barrick North Mara, kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, umeandaa mashindano ya soka ya kuwania kombe la ‘Mahusiano Cup’ yanayojumuisha vijiji 16 vinavyozunguka mgodi huo ambayo yalizinduliwa rasmi jana katika viwanja vya shule ya sekondari ya Ingwe wilayani Tarime.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, Apolinary Lyambiko (aliyesimama) akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mashindano hayo

Mashindano haya yenye kauli mbiu ya “Mahusiano bora kwa uwekezaji Endelevu” yaliwashirikisha wananchi kutoka vijiji mbalimbali na wafanyakazi wa Barrick North Mara, ambapo waliburudika kwa kucheza michezo ya aina mbalimbali. Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Tarime, Kanali Michael Mtenjele, aliyeongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali wilayani humo.

Vijiji ambavyo timu zake zinashiriki katika mashindano hayo ni Genkuru, Msege, Komarera, Nyamwanga, Kewanja, Nyakunguru, Kerende, Nyabichume, Mji Kati, Matongo, Nyangoto, Mrito, Keisangoro na Nyarwana.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kanali Michael Mntenjele (kulia) akizungumza na timu za Kewanja FC na Mosege FC wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko, alisema michezo ni nyenzo muhimu katika kujenga na kudumisha uhusiano katika jamii “Bila mahusiano bora na jamii inayotuzunguka sisi kama kampuni hatuwezi kufanya kazi kwa utulivu,hali ambayo inaweza kusababisha uwekezaji wetu usiletee manufaa katika pande zote mbili”amesema.

Mkuu wa wilaya ya Tarime, Kanali Mntenjele, aliwataka washiriki wa mashindano hayo kucheza kwa amani na wasimamizi husika kutenda haki bila kupendelea timu yoyote.

Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara (kushoto) akishiriki kucheza ngoma ya asili wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo

Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara, ameipongeza Barrick North Mara, kwa kuandaa mashindano hayo,alisema yatahamasisha ushirikiano kutoka kwa jamii inayozunguka Mgodi huo ili kuwezesha kila upande kunufaika.

Wakiongelea kuhusu mashindano haya,baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliipongeza Barrick North Mara, kwa kuleta mabadiliko chanya mbalimbali kupitia uwekezaji wake ikiwemo kuwapatia wananchi burudani kupitia mabonanza ambayo yamekuwa yakiandaliwa na kufadhiliwa na mgodi huo.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kanali Michael Mntenjele, (mwenye kofia) akikagua timu ya waamuzi wakati wa uzinduzi wa mashindano ha
Wananchi wakishiriki mashindano ya kuvuta kamba wakati wa uzinduzi huo
Wananchi wakishiriki mashindano kukimbiza kuku wakati wa uzinduzi huo
Wananchi wakishiriki mashindano kukimbia kwa maguni wakati wa uzinduzi huo

By Jamhuri