Habari MpyaBarrick, Polisi washiriki matembezi ya kupinga vitendo vya ukatili Dar Jamhuri1 year ago1 year ago02 mins Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za wilaya ya Kinondoni na wananchi wakishiriki matembezi ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi ikiwa ni maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wanafunzi walioshiriki katika matembezi ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Barrick kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo na Maofisa kutoka Jeshi la Polisi. Meneja wa Barrick nchini Tanzania,Georgia Mutagahywa,akiongea na washiriki wa maandamano yakupinga vitendo vya ukatili yaliyofanyika jana jijini yaliondaliwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi dawati la jinsia.Wengine pichani ni Maofisa kutoka Jeshi la Polisi na Serikali Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Stella Msofe (kushoto) akiongea wakati wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto yaliyoandaliwa na Kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Dawati la jinsia la Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaaam yaliyofanyika jana katika viwanga vya kituo cha Polisi cha Oysterbay. Katikati ni Meneja wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa na Kamishna Msaidizi wa Polisi( ACP) Alyoce Nyantora ambaye alimwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP, Camilius Wambura Post Views: 5 Post navigation Previous: Kipigo cha Ihefu, kimewapeleka Yanga kwenye presha sahihiNext: Bocco aivuruga Simba
RC mpy Shinyanga ataka elimu itolewe kwa wananchi kuacha kucheza kamali Jamhuri9 hours ago9 hours ago 0
Mbarawa aridhishwa na majaribio ya safari ya treni ya SGR kipande cha Dar hadi Moro Jamhuri13 hours ago 0