Category: Uchumi
Maswi: Kila Mtanzania atapata umeme
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imesema umeme ni huduma ya lazima kwa Watanzania na itafanya kila liwalo kuhakikisha kila Mtanzania anapata umeme. Msimamo wa Serikali umetolewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wakati akizungumza katika kipindi cha Tuambie kupitia runinga ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), wiki iliyopita.
Muhongo akagua ujenzi bomba la gesi
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ameeleza kuridhishwa kwake na kasi ya utandazaji na uunganishwaji wa mabomba ya kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
Matapeli wakubwa Tanzania hadharani
RIPOTI MAALUM
*Watumia madini kutapeli Wazungu hadi bilioni 160/-, watamba
*Mwanza, Dar, DRC, Zambia, Papa Msofe, Aurora waongoza ‘jeshi’
*BoT, NBC, Exim Bank, Polisi, Mahakama, Uhamiaji nao watumika.
Baada ya sifa ya Tanzania kuingia doa kutokana na watu wengi maarufu kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, uchunguzi wa JAMHURI umebaini kuwa matajiri wengi nchini wanatuhumiwa kufanya utapeli wa kutupwa kwa Wazungu kupitia ahadi hewa za kuwauzia madini.
Mtendaji mkuu Osha alalamikiwa Tughe
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Dk. Akwilina Kayumba, amelalamikiwa mbele ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), kuwa anawaongoza kimabavu wafanyakazi wa taasisi hiyo ya Serikali.
UNESCO, WHC wakubali barabara NCAA-SENAPA
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kituo cha Urithi wa Dunia (WHC) wameikubalia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ifanye upembuzi yakinifu wa barabara ya Lodoare-Serengeti.
Wanaume watelekeza watoto walemavu Arumeru
*Wanawake wasukumiwa mzigo
Tatizo la wanaume kuwatelekeza watoto wao wenye ulemavu, limetajwa kukithiri katika Kijiji cha Ambureni, Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.