JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Wakataa maji wakidai hawakushirikishwa

Wakazi wa Kitongoji cha Mkulila, Kijiji cha Wambishe wilayani Mbeya, wamekataa mradi wa umwagiliaji maji waliopelekewa na Serikali, wakidai hawakushirikishwa katika uanzishwaji wake.

Kibanda alivyotekwa

Mfanyakazi wa Kampuni Ikolo Investiment Ltd, Joseph Ludovick (31), aliyekamatwa na Polisi akihusishwa kwenye sakata la utekaji na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, anatajwa kuwa ni mtu muhimu katika upelelezi wa tukio hilo.

Haki za wanawake zitambuliwe kwenye Katiba

Haki ya mwanamke ni suala linalohitaji kupewe umuhimu wa kipekee katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ujasiriamali waajiri vijana 3,000 Arusha

 

Wahitimu zaidi ya 3,000 wa mafunzo ya ujasiriamali katika taasisi ya The Fountain Justice Training College ya jijini Arusha, wameweza kujiajiri na hivyo kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.

Ushindi wa Uhuru Kenyatta ulivyopokewa Kenya

Wafuasi wa Uhuru Kenyatta walijitokeza mwishoni mwa wiki kusherehekea ushindi wake wa kiti cha urais wa Kenya. Uhuru amepata ushindi kwa asilimia 50.03 dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Raila Odinga.

Siri za nyumba za mawaziri zavuja

*Baadhi wadaiwa ‘kuzikacha’

Matumizi ya nyumba za mawaziri jijini Dar es Salaam yamegubikwa na siri nzito. Inadaiwa kuwa baadhi ‘wamezitosa’ kwa kisingizio cha kukosa usiri.