Category: Kitaifa
Wakubwa wanavyotafuna Bandari
Majambazi wajitangazia Serikali
*Wajiundia Jeshi la Ukombozi la Wana Sonjo
*Wabuni bendera, mahakama na polisi yao
*Vijiji vyawatii, waendesha ujangili, ujambazi
Watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 500 wanaodhaniwa kuwa ni majambazi na majangili, wamejiundia serikali ndani ya Msitu wa Igombe mkoani Tabora, JAMHURI inathibitisha.
Wamejiundia uongozi madhubuti pamoja na jeshi walilolipa jina la Jeshi la Ukombozi la Wana Sonjo.
Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa huenda idadi ya watu hao ikawa kubwa kuliko inavyodhaniwa, kwani wanadaiwa kusambaa ndani ya misitu minene katika mikoa ya Tabora na Shinyanga. Pia wapo katika maeneo kadhaa ya Mkoa wa Kigoma.
Imebainika kuwa watu hao wapo katika Msitu wa Igombe uliopo wilayani Uyui na kusambaa katika mapori mengine ya Malagarasi na Myowosi; na walianza kujiimarisha tangu mwaka 2010.
Duru za uchunguzi zimebaini kuwa wanaounda ‘serikali’ hiyo wanatoka katika makabila kadhaa ya mikoa ya Tabora, Shinyanga, Arusha, Kigoma na katika mataifa jirani, hasa Burundi.
“Serikali” hiyo batili ina jeshi lake la ulinzi, jeshi la polisi, mahakama na vyombo vingine vya utawala.
Shughuli kuu zinazofanywa ni ujambazi, ujangili, kilimo cha bangi, biashara ya mbao, uuzaji bunduki pamoja na risasi; na uhalifu wa aina nyingine.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwasa, amezungumza na JAMHURI na kusema, “Ni kweli tuna tatizo hilo. Lipo na ni kubwa. Serikali imeshalitambua, na hatua zinachukuliwa.”
Mwasa, licha ya kukiri, hakutaka kuingia kwenye undani wa suala hilo katika kile kinachoonekana kuwa ni kutotaka kutibua hatua za kiusalama zilizopangwa kuchukuliwa na vyombo vya dola katika kukabiliana na genge hilo.
Hata hivyo, maneno ya Mwasa katika kuthibitisha ukubwa wa jambo hili ni haya, “Kweli tatizo lipo…ni kubwa kuliko unavyofikiri.”
Watu wawili waliokamatwa na baadaye kutoroka kutoka mikononi mwa kundi hilo wamesema genge hilo ni masalia ya wale walioshughulikiwa na Serikali mwaka 2010. Majina ya watu hao tunayahifadhi kutokana na sababu za usalama wao.
“Kuna jeshi lenye askari wa jadi wenye bunduki za SMG (Sub Machine Gun), na magobore. Wanaendesha uasi. Wamepandisha bendera ya bluu, imeandikwa Jeshi la Ukombozi la Wana Sonjo. Wahalifu wengi wageni wanatoka Burundi. Wanashirikiana na Wasonjo, Wasukuma na Waha.
“Shughuli zao ni kilimo cha bangi, kupasua misitu, uwindaji haramu na n.k. Wana watemi wao. Kila mtemi analindwa na askari wasiopungua 20,” anasema mmoja wa watoa habari wetu.
Uimara wa magenge hayo ya wahalifu yaliyojiimarisha yamewafanya hata wananchi na viongozi wa vijiji jirani na mapori wanamoishi, wawe watiifu kwao.
“Ukiwa na tatizo unaenda msituni kuomba msaada wa askari kukukamatia mhalifu au mbaya wako. Wanatumwa askari wanakuja kukuteka na kukupeleka huko msituni.
Bandari Dar inakufa
*Mkurugenzi Mkuu Kipande aingiza ukabila, udini, majungu
*Wafanyakazi watatu bandarini wafariki kutokana na vitisho
*CCTV hazifanyi kazi tangu 2011, wachonga dola mil. 6.5
*Mnikulu Gurumo, Mtawa wampa kiburi, wachafua jina la JK
*Amdanganya Dk. Mwakyembe, amtukana Balozi wa Japan
Kuna kila dalili kuwa Bandari ya Dar es Salaam inakufa kutokana na uongozi mbovu uliojiingiza katika majungu, udini, ukabila na majivuno yasiyo na tija. Wafanyakazi katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wamepoteza morali wa kufanya kazi kutokana na vitisho na matusi ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Madeni Juma Kipande.
Hadi habari hii ya kiuchunguzi inachapishwa wafanayakazi watatu; Peter Gwamaka Kitangalala, Dotto Mbega na mwingine aliyefahamika kwa jina la Lyochi wamefariki dunia katika kipindi cha miezi mitatu kutokana na shinikizo la damu lililozaa kiharusi baada ya vitisho vya Kipande.
Katika hali ya kuwavuruga wafanyakazi wa bandari, Katangalala alihamishiwa Mwanza na baada ya miezi miwili akahamishwa tena kwenda Lindi, huku akipewa vitisho kuwa muda wowote ajiandae kufukuzwa kazi. Kutokana na hofu, alipata kiharusi (stroke) akafa. Mbega kwa upande wake yeye alikuwa makao makuu Dar es Salaam, lakini kutokana na vitisho vya kila siku vya Kipande na wasaidizi wake, naye akapata kiharusi mwezi mmoja uliopita akafariki dunia.
Jumapili ya Machi 30, mfanyakazi mwingine aliyefahamika kwa jina moja la Lyochi huku wengine wakisema ni Oluwochi mwenye asili ya Wajaruo, aliyehamishiwa bandari ya Kasanga, Sumbawanga naye aliaga dunia kwa ugonjwa huo huo wa kiharusi kutokana na mashinikizo ya Kipande.
“Uhalisia hali inatisha. Kipande anajinadi kuwa atamfukuza kila mtu, na kweli anafukuza anaajiri watu wa dini yake. Kuna kabila la Wahaya kutoka Kanda ya Ziwa, hilo utadhani waliwahi kushikana nalo ugoni. Mhaya yeyote aliyemkuta kazini ameapa kumg’oa. Amehamisha [Hassan M.] Kyomile kwa sababu ya kabila lake na kwamba aliomba kazi ya Ukurugenzi Mkuu,” kilisema chanzo chetu.
Kyomile amehamishwa Machi mwaka huu, kutoka makao makuu alikokuwa Mkurugenzi wa Ununuzi na kwenda kuwa Meneja wa Bandari Tanga.
Nyalandu ‘auza’ Hifadhi
*Yeye, James Lembeli waenda Afrika Kusini kukamilisha mpango
*Baada ya Katavi Hifadhi nyingine nazo zitatolewa kwa wawekezaji
*Katibu Mkuu ashinikizwa, abaki njia panda kuidhinisha safari, malipo
*Urafiki wa Waziri, Lembeli waibua shaka miongoni mwa watumishi
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, yupo kwenye hatua za mwisho za kuikabidhi Hifadhi ya Taifa ya Katavi kwa mwekezaji wa Afrika Kusini.
Bilionea Lake Oil kitanzini
*Yeye, wenzake wafungiwa vituo kwa kuchakachua *Walipa mamilioni ya shilingi Kampuni ya Lake Oil inayomilikuwa na bilionea Ally Awadh, imeingia matatani baada ya vituo vyake vinne vya mafuta kufungiwa kutokana na kuuza mafuta yasiyokuwa na vinasaba. Vituo vilivyofungwa ni Lake…
Ufisadi wa kutisha Mamlaka ya Ngorongoro
*Mapato ya Sh milioni 300 yaingia mifukoni *Safari hewa zagharimu shilingi bilioni 1.316 *Bia, soda, teksi vyagharimu Sh milioni 133 *Masurufu pekee yalamba shilingi milioni 100 Ufisadi wa kutisha umebainika kuwapo katika Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro (NCAA), huku Serikali…
- TANESCO yazindua rasmi zoezi la ulipwaji fidia kwa wananchi Lindi na Mtwara
- CRDB yaendelea kung’ara katika uwekezaji wa kimkakati Soko la Hisa DCE
- Rais Samia anaendelea kupeleka furaha na neema kwa watumishi wa umma Tanzania – Kikwete
- Polisi yamkamata mmiliki wa eneo la Vikawe lililosababisha vifo vya watu wawili
- Chem Chem Safari ya Tanzania yaingia katika ushirikiano na Auberge, wadhamiria kulinda mazingira
Habari mpya
- TANESCO yazindua rasmi zoezi la ulipwaji fidia kwa wananchi Lindi na Mtwara
- CRDB yaendelea kung’ara katika uwekezaji wa kimkakati Soko la Hisa DCE
- Rais Samia anaendelea kupeleka furaha na neema kwa watumishi wa umma Tanzania – Kikwete
- Polisi yamkamata mmiliki wa eneo la Vikawe lililosababisha vifo vya watu wawili
- Chem Chem Safari ya Tanzania yaingia katika ushirikiano na Auberge, wadhamiria kulinda mazingira
- Legendary Expeditions, yaingia mkataba wa ushirikiano na kampuni ya Auberge Collection
- Jaji Mkuu Masaju kuzindua kitabu cha Ushairi cha Wakili Msomi Aisha Kingu Jumapili
- Dodoma yapongezwa kwa mpango wa kupeleka walimu Korea Kusini
- Waziri Mkuu: Serikali yaendelea kuhakikisha mafuta hayaadimiki nchini
- Vyuo 263 vya ufundi kusajiliwa kuongeza fursa za mafunzo ya ufundi
- IPI yawateua mabalozi 500 wa kuitangaza amani ndani na nje ya nchi
- EWURA CCC Kagera yafanikiwa kuwafikia wananchi 1134
- TANESCO yapongezwa kujipanga kufikisha umeme Bandari ya Uvuvi Kilwa
- Dk Jingu apokelewa Wizara ya Katiba na Sheria, aahidi ushirikiano
- Benki ya MCB yazindua mpango wa uuuzaji wa hisa stahiki