JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Magufuli amvimbia Pinda

Kuna kila dalili kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli, amekataa au kushindwa kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutokana na kilichoelezwa kuwa kuyatekeleza ni kuvunja sheria ya usalama barabarani na kanuni zake, hivyo yeye hayuko tayari kufanya hivyo.

PPF yafafanua michango ya zamani

Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF) umewatoa wasiwasi wafanyakazi wa mashirika ya umma waliochangia tangu mwaka 1978, kwa michango isiyoonekana kwenye mtandao wa mfuko huo.

TEF, MCT wampongeza Kikwete

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Baraza la Habari Tanzania (MCT) wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua ya kutangaza akiwa jijini London kuwa kuanzia mwakani, Serikali itatunga Sheria ya Haki ya Kupata Habari.

Chadema ‘Kimewaka’

Chimbuko migogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unasababishwa migongano wa kupata madaraka ndani ya chama hicho, JAMHURI limebaini

Imelezwa kuwa mtafaruku uliotokea mwishoni mwa wiki na kusababisha kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa  Mkoa wa Arusha wa Chadema  kwa muda usiojulikana ni mgongano wa kutafuta madaraka ndani ya chama hicho.

‘Majangili’ 20 hatari

  • JWTZ watisha, maofisa Maliasili 16 wakamatwa
  • Mmoja akutwa anamiliki bunduki 5 za rifle kali
  • Mbunge Mtutura ahojiwa, Nchambi naye atajwa
  • RCO aliahidiwa dola 3,000 akawaachia Waarabu

Operesheni Tokomeza inayoendeshwa chini ya usimamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), imewakamata watumishi kadhaa wa Serikali wanaotuhumiwa kujihusisha na ujangili. Operesheni hiyo inaongozwa na Luteni Kanali A. Sibuti.

Rushwa yazigonganisha Mahakama, Wizara

Wizara ya Nishati na Madini imeingia kwenye mvutano na Mahakama baada ya mhimili huo kuamuru raia wa China aliyekamatwa akitorosha madini ya tanzanite, arejeshewe madini hayo kinyume cha sheria.