JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

UNESCO, WHC wakubali barabara NCAA-SENAPA

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kituo cha Urithi wa Dunia (WHC) wameikubalia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ifanye upembuzi yakinifu wa barabara ya Lodoare-Serengeti.

Rwanda: Kagame hakumtukana Kikwete

*Yawataka Watanzania kupuuza uvumi mitandaoni

Baada ya kuwapo joto kali la maneno ya kidiplomasia kutoka kwa maafisa wa Serikali za Tanzania na Rwanda kutokana na habari kwamba Rais wa Rwanda, Paul Kagame amemtukana Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, Serikali ya Rwanda sasa imetoa msimamo rasmi kukanusha tuhuma hizo.

Chikawe: Tume ya Katiba ipokee maoni, isijibu

Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe ameitaka Tume ya Mabadiliko ya Katiba kusikiliza zaidi maoni ya wananchi na kuyapokea badala ya kuyajibu kila yanapotolewa.

Madiwani Chadema Geita wafichua ufisadi wa bil 11/-

*Tamisemi, Hazina, CCM wahusishwa

Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa Halmashauri ya Mji wa Geita, kwa kushirikiana na mmoja wa Viti Maalum wa Halmshauri ya Wilaya ya Geita, wametoa nyaraka katika mkutano hadhara uliofanyika Julai 14, mwaka huu, zinazoonesha wilaya hiyo kupokea Sh bilioni 11 kwa ajili ya ununuzi wa madawati lakini matumizi yake hayajulikani.

Wasira: Nivigumu kuifuta Chadema

*Akiri kuwa kazi hiyo si nyepesi

Kukifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) si rahisi; amethibitisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.

Wanaume watelekeza watoto walemavu Arumeru

*Wanawake wasukumiwa mzigo

Tatizo la wanaume kuwatelekeza watoto wao wenye ulemavu, limetajwa kukithiri katika Kijiji cha Ambureni, Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.