Category: Kitaifa
Wasira: Nivigumu kuifuta Chadema
*Akiri kuwa kazi hiyo si nyepesi
Kukifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) si rahisi; amethibitisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.
Wanaume watelekeza watoto walemavu Arumeru
*Wanawake wasukumiwa mzigo
Tatizo la wanaume kuwatelekeza watoto wao wenye ulemavu, limetajwa kukithiri katika Kijiji cha Ambureni, Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.
Ulaji ugeni wa marais 11
Kampuni ‘hewa’ zakomba mamilioni
*CAG atakiwa aingie kazini mara moja
Kampuni tatu kati ya nane zilizozawadiwa zabuni tata za vifaa na huduma kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), zimebainika kuwa ni ‘hewa’.
Waziri Mku: Tutavuna gesi asilia baada ya miaka kumi
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema mavuno ya gesi asilia iliyopo mkoani Mtwara yataanza kupatikana baada ya kipindi kisichopungua miaka kumu.
Nchi imetafunwa!
*Hazina yatumia Shilingi bilioni 8, taasisi za umma
zachangishwa, ‘wajanja’ watafuna mamilioni
*Vifaa vya Obama vyaokoa jahazi, sare, mikoba, vyagharimu
mil. 400/-, vinyago navyo balaa!
*Karamu, chupa za kahawa, miavuli mil. 390/-,
Burudani ya muziki yatafuna milioni 195/-
*Dewji agoma kuchangia, Katibu Mkuu Haule
arushiwa kombora, yeye ajitetea
Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), uliomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, umeigharimu Serikali Sh bilioni nane.
Sakata la Iddi Simba bado bichi
*Ikulu, ofisi ya CAG washangazwa kuachiwa
*Uamuzi uliofanywa na DPP wazua maswali
Kuachiwa kwa mwanasiasa Iddi Simba, ambaye hivi karibuni alikuwa akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kabla ya Mkurugenzi wa Mshitaka nchini (DPP), kuamuru awe huru, kumeibua mgongano mkubwa serikalini.