Category: Kitaifa
Polisi matatani tena
JESHI la Polisi limeingia matatani kwa kumtangaza ‘mbaya wao’ aliyeibua kile alichodai kwamba ni mtandao wa uhalifu na mauaji ndani ya Jeshi hilo mkoani Mwanza, kwamba ni kichaa.
Mauaji ya Barlow wingu zito latanda
*Polisi wasema kijana aliyetaja mtandao ni mgonjwa wa akili
*Yeye asisitiza kuwa kichaa, analazimishwa dawa Muhimbili
*Ndugu waeleza historia, daktari anayemtibu aingia mitini
Jeshi la Polisi nchini limempeleka na kumlaza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kijana Mohamed Malele, mshirika wa mtandao uliohusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, wakidai ni mgonjwa wa akili.
RPC ‘atumika’ kuchangisha rushwa
* Watendaji wadaiwa kutumia jina lake kula rushwa kwa walima bangi
* RPC Tarime/Rorya awaruka, DC asema dawa yao inachemka
Maofisa watendaji wa Kijiji cha Kwisarara na Kata ya Bumera wanatuhumiwa kutumia jina la Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) wa Kipolisi Tarime/Rorya kuchukua rushwa ya fedha kutoka kwa wakulima wa zao haramu la bangi.
Diwani awaangukia wezi wa sola
Diwani wa kata ya Kisaka wilayani Serengeti, Chacha Togoche, ‘amewangukia’ wezi akiwaomba kutorudia kuiba sola katika zahanati ya kijiji cha Nyiboko.
JWTZ kuleta amani DRC-Membe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, amesema anaamini kuwa msimamo na uamuzi wa kupeleka kikosi cha kulinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) utaleta amani ya kudumu nchini humo.
Serikali yamkaanga raia wa Uswiss
. Yamnyang’anya umiliki wa ardhi aliyojipatia kinyemela
. Aliitumia kuuza viwanja kwa wageni kinyume cha sheria
. Raia wa Zimbabwe alishauziwa na kujenya nyumba
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imemnyang’anya raia wa Uswiss umiliki wa ardhi mkoani Tanga.