Category: Kitaifa
Vita kubwa TANESCO
*Wabunge wajiandaa kukwamisha tena bajeti ya Wizara ya Nishati, wahoji zabuni ya mafuta BP
*Wajiandaa kuwang’oa Waziri Profesa Muhongo, Katibu Mkuu Maswi Ijumaa ya wiki hii
*Katibu Mkuu aanika ukweli, asema Wizara yake haikufanya manunuzi waliohusika ni RITA, Zitto anena
[caption id="attachment_219" align="alignleft" width="243"]
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo[/caption]Kuna kila dalili kuwa imeibuka vita ya wazi kati ya Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), huku Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, William Mhando, akipigiwa debe la wazi na wabunge.
Taarifa zilizopatikana kwenye ofisi za Bunge zinasema kuwa Kamati ya Nishati na Madini inajipanga kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kama Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, Injinia Mhando, hatarejeshwa kazini huku wizara ikisisitiza kuwa amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wala hajafukuzwa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, naye ana msimamo kuwa Mhando ameonewa na wizara inaweza kujiokoa kwa kumrejesha ofisini kisha ufanywe uchunguzi maalumu utakaoendeshwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
Ufisadi watikisa Bunge
*Unahusu kada wa CCM anayechimba urani
*Profesa Tibaijuka amtwika mzigo Jaji Werema
*Naibu Spika aagiza Waziri Muhongo ajiandae
*Sinema nzima imeibuliwa na Halima Mdee
Wafanyabiashara ndugu wanaodaiwa kubadili matumizi ya ardhi kutoka uwindaji wa kitalii na kuanza harakati za uchimbaji madini ya urani, wameibua mgongano mkubwa bungeni na serikalini. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amemwomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, asaidie kupata utatuzi kashfa hiyo.
Hotuba ya Lissu iliyolitikisa Bunge, Serikali
*Atoboa siri majaji wengi ‘vihiyo’, washindwa kuandika hukumu
*Aeleza namna wakuu wa wilaya walivyoteuliwa kwa rushwa
*Yumo mwingine aliyehukumiwa kwa ubaguzi wa ukabila
Ifuatayo ni sehemu ya maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu, kuhusu Mpango wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha wa 2012/2013. Lissu alitoa maoni haya na kwa kiasi fulani yaliibua mjadala mkali bungeni, huku Serikali ikitaka aondoe baadhi ya maneno, na yeye akakataa. Endelea…
UTEUZI WA MAJAJI
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inatambua ukweli kwamba Rais Kikwete ameteua majaji wengi wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano kuliko marais wengine wote waliomtangulia kwa ujumla wao. Rekodi hii peke yake inaonyesha kwamba Rais anatambua umuhimu wa Mahakama Kuu kuwa na watendaji wa kutosha wa utoaji haki ili kutekeleza dira ya ‘haki kwa wote na kwa wakati.’
‘Majaji ndiyo waliomtuma Lissu’
Hotuba kali ya Tundu Lissu ya kukosoa uteuzi wa majaji dhaifu uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete, imeelezwa kwamba ina baraka zote za baadhi ya viongozi waandamizi wa Mhimili wa Mahakama, JAMHURI limeelezwa.
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
DIRA YA WIZARA:
Kuwa na uhakika wa milki za ardhi, nyumba bora na makazi endelevu kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
DHIMA:
Kuweka mazingira yanayofaa kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma za ardhi, nyumba na makazi
- ACT yaomba Serikali ipunguze tozo kutokana hali ya maisha
- Waziri Kapinga : Ushirikiano wa Tanzania na EU ufungue milango ya kiuchumi na sio utegemezi
- CHADEMA Pwani yataka maeneo ya umma yapimwe kuepusha migogoro ya ardhi
- TANESCO yazindua rasmi zoezi la ulipwaji fidia kwa wananchi Lindi na Mtwara
- CRDB yaendelea kung’ara katika uwekezaji wa kimkakati Soko la Hisa DCE
Habari mpya
- ACT yaomba Serikali ipunguze tozo kutokana hali ya maisha
- Waziri Kapinga : Ushirikiano wa Tanzania na EU ufungue milango ya kiuchumi na sio utegemezi
- CHADEMA Pwani yataka maeneo ya umma yapimwe kuepusha migogoro ya ardhi
- TANESCO yazindua rasmi zoezi la ulipwaji fidia kwa wananchi Lindi na Mtwara
- CRDB yaendelea kung’ara katika uwekezaji wa kimkakati Soko la Hisa DCE
- Rais Samia anaendelea kupeleka furaha na neema kwa watumishi wa umma Tanzania – Kikwete
- Polisi yamkamata mmiliki wa eneo la Vikawe lililosababisha vifo vya watu wawili
- Chem Chem Safari ya Tanzania yaingia katika ushirikiano na Auberge, wadhamiria kulinda mazingira
- Legendary Expeditions, yaingia mkataba wa ushirikiano na kampuni ya Auberge Collection
- Jaji Mkuu Masaju kuzindua kitabu cha Ushairi cha Wakili Msomi Aisha Kingu Jumapili
- Dodoma yapongezwa kwa mpango wa kupeleka walimu Korea Kusini
- Waziri Mkuu: Serikali yaendelea kuhakikisha mafuta hayaadimiki nchini
- Vyuo 263 vya ufundi kusajiliwa kuongeza fursa za mafunzo ya ufundi
- IPI yawateua mabalozi 500 wa kuitangaza amani ndani na nje ya nchi
- EWURA CCC Kagera yafanikiwa kuwafikia wananchi 1134
Copyright 2025
Cookie Consent
We use cookies to improve your experience on our site. By using our site, you consent to cookies.
Cookie Preferences
Manage your cookie preferences below:
Essential cookies enable basic functions and are necessary for the proper function of the website.

