Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.

 

Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

 

Kufanyika kwa kikao hicho kulikuwa ni maandaizi ya kuwaweka sawa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi, waweze kuipitisha bajeti hiyo. Hilo ni jambo la kawaida katika mabunge, hasa yenye mseto wa wabunge wanaotokana na vyama vingi vya siasa.

Read More

Tujiepuke bejeti kiinimacho

Wiki hii Serikali inatarajiwa kuwasilisha bajeti bungeni mjini Dodoma. Bejeti hii inakisiwa kuwa ya wastani wa shilingi trilioni 15. Hili ni ongezeko la wastani wa trilioni 2 kutoka trilioni 13 za mwaka jana. Kiasi hiki ni kikubwa mno kwa takwimu. Kinawafanya Watanzania kuwa na matumaini makubwa ila yapo yanayotusikitisha.

Read More