Category: Maoni ya Mhariri
Wachochezi wa vurugu waadabishwe ipasavyo
Wiki iliyopita, Jeshi la Polisi lilitangaza kumtia mbaroni mtu anayedaiwa kuwa kinara wa kusambaza ujumbe wa kuchochea chuki na uhasama hapa nchini, kupitia simu za kiganjani.
Vurugu za Mtwara ni uhuni na upuuzi
Kwa mara nyingine, wahuni kadhaa katika Mji wa Mtwara jana waliendesha vitendo vya uvunjifu wa amani. Watu kadhaa wameripotiwa kuuawa, kujeruhiwa na mali za mamilioni ya shilingi zimeteketezwa.
Polisi wachunguze tuhuma hizi
Habari kubwa katika toleo la leo inahusu mtandao wa mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza Liberatus Barlow. Ndani ya habari hiyo, gazeti hili la JAMHURI linamtaja mtuhumiwa Mohamed Edward Malele, Mkazi wa Kijiji cha Igoma, Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza anayekisiwa kuwa na umri wa kati ya miaka 30 hadi 40 kuwa anashikiliwa na dola.
Dk. Kawambwa mtuhumiwa Na 1
Wiki iliyopita tuliandika maoni tukichagiza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aanzishe mchakato wa kufukuzwa kazi katika Baraza la Mitihani Tanzania, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Joyce Ndalichako. Tulisema uamuzi wa Baraza la Mitihani (NECTA) kubadili mfumo wa kuchakata matokeo na kufanya wanafunzi wengi kushindwa hauvumiliki.
Pinda mfukuze kazi Ndalichako
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi, wiki iliyopita amelitangazia Bunge uamuzi mgumu wa Serikali. Ametangaza kuwa Serikali sasa imeamua kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa 2012. Katika mtihani huo wanafunzi asilimia 65.5 walipata daraja sifuri.
JWTZ wakiamua watamaliza ujangili
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imetaka bayana kwamba ujangili ni janga la kitaifa. Hatuhitaji mtaalamu wa utabiri aje kutoa kauli nyingine tofauti na hiyo.