Category: Siasa
Ufwiliku huu wa nini?
Septemba 18, mwaka huu wa 2014 historia ilijirudia katika nchi yetu hii. Nasema hivi kwa sababu Kiongozi Mkuu wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani nchini (CHADEMA), Mheshimiwa Freeman Mbowe alitiwa msukosuko wa kihistoria.
Jifunze kuwa mteja bora
Mara nyingi tumekuwa tukieleza na kuwasisitiza wauzaji wawe na ukarimu kwa wateja (customer care), lakini tumekuwa tukiipuuza nafasi ya mteja katika kumsaidia muuzaji awe mkarimu kwake.
VITA DHIDI YA UJANGILI Waraka muhimu wa Mch. Matwiga …1
Ndugu Watanzania wenzangu na Wizara ya Maliasili na Utalii, kwanza naomba kusema jambo moja kama Mtumishi wa Mungu, ambaye nimeitwa naye kwa maslahi ya mbingu, ili kuijenga jamii na umma kimaadili. Nitasimama siku zote katika “kweli” na hiki ndicho “kiapo changu” ee Mungu tusaidie.
Wamiliki mabasi wana wajibu wa kupunguza ajali
Tatizo la ajali za barabarani limekuwa ni moja ya changamoto kubwa sana katika sekta ya usafiri wa barabara hapa nchini. Katika kipindi cha mwanzo wa mwezi Septemba, 2014 kumetokea ajali za barabarni kubwa zaidi ya mbili katika mikoa ya Mara na Tabora, ambako watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.
Ukweli kuhusu elimu ya Lembeli
Mwalimu Julius Nyerere, ambaye Mheshimiwa James Lembeli amewahi kujifananisha naye, aliwahi kusema kuwa ikitokea mtu wa kawaida akampiga mkewe hadharani, hii haiwezi kuwashughulisha watu na wala haiwezi kuwa habari. Lakini ikatokea yeye (Mwalimu) akafanya hivyo, basi hiyo itakuwa habari kubwa mno.
Mwalimu Nyerere na mgombea binafsi
Mei Mosi, 1995 Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akiwa mgeni rasmi kwenye Sherehe za Mei Mosi mjini Mbeya, alizungumza mambo mengi yaliyolihusu Taifa. Miongoni mwa mambo hayo ni haki ya kuwapo mgombea binafsi. Rasimu ya Katiba Mpya (ya Jaji Warioba) ilizingatia jambo hili muhimu. Hata hivyo, Bunge Maalum la Katiba (katika Rasimu ya Samuel Sitta) limeminya mno haki ya kuwapo mgombea binafsi. Ilivyo ni kama haki hiyo haipo kwani imewekewa vizingiti vizito mno. Soma maneno haya ya Mwalimu Nyerere.